Habari za Punde

Wanawake wengine wamekuwa ni sehemu kuwa katika kutoa mchango wa kuleta mabdiliko ya maendeleo

 

MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amesema Wanawake wengine wamekuwa ni sehemu kuwa katika kutoa mchango wa kuleta mabdiliko ya maendeleo kwa muda mrefu katika sekta na maeneo mbali mbali hapa Zanzibar kwa miaka mingi sasa.

Mhe. Othman ameyasema hayo huko Ofisini kwake Migombani mjini Zanzibar alipokutana na timu ya Utunzi wa Kitabu  cha Mchango wa wanawake kinachoitwa ‘Nyayo za Wananwake Zanzibar’, iliyoongozwa na Meneja wa Mradi wa Uandishi  wa Kitabu hicho Bibi Hannah MacCarriok kutoka Sweeden.

Amesema kwamba  hapa Zanzibar ipo mifano kadhaa wa kadhaa inayoonesha mchango mkubwa uliotolewa na wanawake katika maeneo na mambo tofauti ambao umechangia kuleta manufaa na maslahi makubwa kwa jamii jambo ambalo linaonesha uwezo na umahiri walionao wanawake wengi nchini .

Amesema kuwepo mchanganyiko wa maisha na utamaduni wa  watu kutoka makabila tofauti hapa Zanzibar imesaidia sana wanawake kutoa mchango wao katika harakati za kupatikana haki na maendeleo kwa jamii kwennye Nyanja tofauti.

Mhe. Othman amefahamisha kwamba jamii inapaswa ifahamu kwamba maendeleo bora ya familia yanahitaji kuwepo wanawake mahiri, kwa kuwa ni wenye uthubutu na wanaweza kujenga ushawishi katika kubuni na kutekeleza makakati  na mipango tiofauti ya maendeleo yao na jamii kwa jumla.

Amewapongeza washiriki wa Utunzi wa Kitabu hicho ambacho kimechukua muda wa miaka mitatu kukamilika na kueleza kwamba  wamesaidia kuionesha jamii juu ya suala kubwa la mchango wa wanawake katika maeneo mbali mbali.

Mhe. Othman amewataka watunzi hao kuangalia maeneo zaidi ili kupanua wigo mpana katika kukifanyia mapitio na hatua ya utoaji wa toleo la pili la kitabu hicho ili kuongeza mambo mengi zaidi ya mchango wa wanawake yatakayoanishwa kwenye kitabu hicho.

Naye Meneja wa Mradi wa Utunzi na uandikaji wa kitabu hicho Bibi Hannah MacCarriok, amesema kwamba mchango wa mabadiliko katika jamii unaweza kufanywa na wanawake kutoka katika ngazi zote ndani ya jamii.

Aidha amesema kwamba kitabu hicho mbali na kuonesha machango wa wanawake mbali mbali, lakini pia kinalenga kuonesha na kuwashajiisha wananawake katika kuwajengea uwezo na uthubutu wa kushiriki katika masuala mbali mbali muhimu kwa maendeleo yao na taifa kwa jumla kama walivyofanya wengine.

 

Mwisho.

Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia Kitengo chake cha Habari leo tarehe 02.02.2023.

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.