Habari za Punde

Fanya Juhudi za Kuzisambaza Vyema Taarifa za Matokeo ya Sensa ya Watu na Makaazi Kuzisambamba na Kuhamasisha Taasisi za Serikali na Binafsi juu ya matumizi sahihi ya takwimu hizo

 

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman akipokea vitabu vya taarifa ya matokeo ya Sensa kutoka kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Mipango  Zanzibar Mhe.Dkt.Saada Salum Mkuya, hafla hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza Rais wa Zanzibar Migombani Unguja Jijini Zanzibar.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, ameitika Wizara ya Fedha na Mipango na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu Zanzibar kufanya juhudi za kuzisambaza vyema tarifa za matokeo ya Sensa sambamba na kuhamasisha taasisi za Serikali na Binafsi juu ya matumizi sahihi ya  takwimu hizo kwa kuwa ni fursa muhimu katika kuendeleza kukuza shughuli za kibishara na uchumi nchini.

Mhe. Othman ametoa maelekezo hayo  hayo huko Ofisini kwake Migombani mjini Zanzibar alipokabidhiwa  nakla za vitabu  kumi na moja vya taarifa tofauti za matokeo ya Sensa ya mwaka 2022, kutoka kwa Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar Mhe. Saada Mkuya Salim aliyembatana na Kamisaa wa Sensa Zanzibar Balozi Mohammed Hamza pamoja na Mtakwimu Mkuu wa Serikali Ndugu Salim Kassim Ali.

Mhe. Othman amesema kwamba iwapo taarifa hizo za matokeo ya sense zitatumika ipasavyo zitaweza kuleta manufaa makubwa katika nchi  hasa katika upangaji wa mipango ya maendeleo katika shughuli za kibiashara na toaji wa huduma mbali mbali za kijamii katika ngazi tofauti.

Amesema kwamba jamiii na taasisi za Serikali na binafsi kwa jumla zinahitaji  kuhamasishwa na kuwa na mwamko juu ya kuwepo haja na umuhimu mkubwa wa kutumia taaisfa hizo katika masuala mbali mbali na kuwa chachu ya mabadiliko ya kimaendeleo nchini.

Mhe. Makamu amefahamisha kwamba kufanya hivyo pia ni fursa muhimu kwa serikali katika suala la kuendeleza juhudi za ukusanyaji mapato  hasa kwa vile sense  hiyo imefanywa kwa utaalamu mkubwa uliozingatia masuala muhimu yanayohitajhika katika shughuli za kiuchumi na maendeleo.

Aidha amesema kwamba taasisi zote za serikali ni muhimu kutumia taarifa hizo katika masuala mbali mbali ya mipango na utoaji huduma kwenye sekta na maeneo tofauti jambo litakaloongeza ufanisi na kukuza maendeleo.

Naye Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Saada Mkuya Salim, amesema kwamba kunahitajika juhudi kubwa  kubwa ya kutoa elimu  na kuhamasisha taasisi za serikali ili kuwa na mwamko sahihi wa kuzitumia takwimu zilizopo  katika kuandaa mipango yao mbali mbali.

Aidha Dk. Mkuya amesema pia kuwepo anuani za makazi ( Post Code) kupitia Sensa hiyo  kutasaidia  katika juhudi za Serikali za kuendeleza suala la ukusanyaji wa mapato kwa ufanisi na usahihi zaidi na kuongeza mapato ya serikali.

Kwa upande wake Kamisaa wa Sensa Balozi Mohammed Hamza amsema kwamba  kazi kubwa ya usambazaji wa matokeo ya taarifa za sense inaendelea na kwamba kupatikana kwa taarifa sahihi kupitia anuani za makazi kutasaidia pia kuzuia udanganyifu katika suala zima la ukusanyaji wa mapato.

Wakati huo Mh. Othman amekutana Kamati Mapitio ya sera ya Maji Zanzibar na kueleza kwamba katika muendelezo bora wa sera ya maji ni vyema kuwepo mipango sahihi nay a muda mrefu ya maji sambamba na kufahamu kiwango sahihi cha maji yaliyopo na mahitaji yake kwenye matumizi ili kuwezesha huduma hiyo kutolewa kwa uhakika .

Aidha ameshauri kwamba ni vyema Mamkala ya Maji kuachiwa kazi ya kuitunza rasilimali hiyo ili kuifanya kuwa endelevu na kuwepo chombo kitakachopewa mamlaka na kazi ya kusambaza huduma hiyo kwa watumiaji  huku taasisi zenye mwelekeo mmoja na mnaba wa majukumu kufanya kazi kwa ukaribu zaidi kulimko ilivyo sasa.

Aidha ameshauri kwamba kwa vile kutokana na mamumbile yua Zanzibar arilimali hiyo kutegemnewa zaidi kutoka ardhini ni vyema  kuwepo mpango na mkati  madhubuti zaidi utakaosaidia usimamizi bora wa rasilimali hiyo hasa kwa kuzingatia kwamba kumekuwepo na mabadiliko mkubwa katika maisha ya watu kuishi kisasa zaidi na mahitaji kuwa makubwa kadri siku zinavyokwenda mbele.

Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia kitengo chake cha Habari leo tarehe 07.06.2023

Makamu wa kwanza wa Rais Mhe. Othman Masoud Othman akizungunza na Waziri wa Fedha Mhe, Saada Mkuya (Kulia ) alipofika kumkabidhi Nakla za matokeo ya sena kushoto kwa waziri ni Kamisaa wa sensa Balozi Mhammed Hamza
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman akizungunza na Mkurugenzi wa Sera na utafiti wa Wizara ya Maji Dk. Maryam Issa  alipofika ofisi kwa makamu migombani kupata maoni kuhusu sera  ya mji
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi, baada ya kumalizika kwa hafla ya kukabidhiwa Vitabu vya matokeo ya Sensa ya Watu na Makaazi iliyofanyika mwaka jana na (kushoto kwake) Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar Mhe.Dkt. Saada Salum Mkuya na (kulia kwake) Makamu Mwenyekiti wa Sensa ya Watu na Kakaazi Balozi Mohammed Hamza na Mtakimwi Mkuu DILIYOFA   9 wapili kulia na waziri wa Fedha Saada Mkuya  (kushoto) na kulia kwa makamu ni Balozi Mohammed Hamza na Kushoto kwake ni Mtakwimu Mkuu Salim Kassim Ali

Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia kitengo chake cha Habari leo tarehe 07.06.2023

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.