Habari za Punde

Tanazania inatambua na kuheshimu usawa wa kijinsia kwa kuona umuhimu wa kuwachagua wanawake kwenye mihimili yote ya Serikali - Dk.Mwinyi

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikabidhiwa TUZO Maalum ya kumpongeza,iliyotolewa na Taasisi ya Tanzania Women Cross Party Platform (ULINGO) akikabidhiwa na Makamu Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe.Mgeni Hassan Juma, hafla hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali              Mwinyi amesema Tanazania inatambua na kuheshimu usawa wa kijinsia kwa         kuona umuhimu wa kuwachagua wanawake kwenye mihimili yote ya Serikali,       Bunge na Mahakama kwa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya        Mapinduzi ya Zanzibar.                                                                                                                  

Dk. Mwinyi aliyasema hayo, Ikulu, Zanzibar alipozungumza na uongozi wa taasisi ya kiraia, inayounganisha Jumuiya za wanawake kutoka vyama mbalimbali vya siasa vyenye usajili kamili nchini, tasisi ya Sauti ya wanawake wenye ulemavu (SWAUTA), Chama cha wabunge wanawake (TWPG) na Umoja wa wanawake wa Baraza la Wawakili (UWAWAZA). T-WCP - ULINGO. Waliofika kumkabidhi tunzo ya hongera kwa mafaniko makubwa aliyofanya ndani ya muda mfupi wa uongozi wake.

Alisema serikali zote mbili zitaendelea kutoa fursa za kutosha kwa wanawake kwenye maeneo mbalimbali ili kutekeleza azma yao kufikia 50 kwa 50.

Alisema maendeleo yana taka kwa usawa wakijinsia kutoa haki na fursa sawa katika maendeelo ikiwemo elimu, afya na jamii kwani kumuelemisha mwanamke kutaondoa changamoto nyingi kwenye jamii

“Sijajuta hata kidogo kwa wale wanawake niliowateua kwenye Serikali yangu, kwa kweli naona umuhimu wa kuwaongeza kwenye safu mbalimbali” Alibainisha Rais Dk. Mwinyi.

Aidha, alisema Serikali pia itaendelea kuimarisha huduma za mama na mtoto ili kupunguza changamoto nyingi kwa wanawake.

Rais Dk. Mwinyi pia aliwapongeza ULINGO kwa kazi kubwa wanayoifanya kuunganisha pamoja sauti ya pamoja, na kuwasifu hatua yao ya kutanguliza maslahi mapana ya taifa kwa kuunganisha nguvu ya umoja wao bila kujali tofauti ya itikadi zao za kisiasa pamoja na kuwashirikisha wanawake wengi na kuwashajihisha kitaaluma kujua haki na wajibu wao kwenye masuala haki na siasa.

Alisema, katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania inatoa haki kwa jinsia zote kushiriki katika masuala siasa. Pia Dk. Mwinyi aliahidi kuipokea tunzo hiyo kama sehemu ya kuongeza za kuweka fursa sawa za jinsia kwenye maeneo yote.

Nao, viongozi wa taasisi hiyo wamempongeza Dk. Mwinyi kwa kutekeleza kwa vitendo masuala ya usawa wa kijinsia na ujumuishi wa makundi maalum katika ngazi mablimbali za maamuzi, kulinda na kudumisha amani, umoja na utulivu nchini na kushajihisha umoja wa kitaifa pamoja na masuala ya msingi kwa maendeleo endelevu.

Pia, walimpongeza Rais Dk. Mwinyi kwa kutambua kikwazo kimubwa kinachowanyima fursa wananwake ikiwemo ukosefu wa elimu, changamoto kwenye sekta ya afya kwa kuweka miundombinu imara ili kukabiliana na changamoto pamoja na huzitatua kwa kipindi kifupi cha uongozi wake.

Akizungumza kwenye halfa hiyo kwa niaba ta Mwenyekiti wa taasisi hiyo, Anna Magareth Abdalla, Makamo Mwenyekti wa taasisi hiyo kwa Zanzibar ambae pia ni Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi, Mgeni Hassan alimuahidi Dk. Mwinyi mwaka 2025 atarejeshwa tena madarakani kwa nguvu na umoja wa wanawake nchini ambao kwasasa sauti yao ni moja tu ya kudumisha amani yanchi na maendeleo kwa maslahimapana ya taifa.

Pia alitumia fursa hiyo kumpongeza Dk. Mwinyi kwa kwa mageuzi makubwa aliyoiletea Zanzibar kupitia sekta za Afya, Elimu na Uchumi wa Buluu pamoja na kuongeza fursa za uongozi na maendeleo kwa wanawake na kumuahidi daima wanamuunga mkono katika kuiletea maendeleo makubwa Zanzibar.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Ujumbe wa Uongozi wa Taasisi ya Tanzania Women Cross Party Platform (ULINGO) walipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo na kumkabidhi TUZO Maalum ya kumpongeza, mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar leo 12-6-2023, ukiongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe.Mgeni Hassan Juma.
Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Zena Ahmed Said akiwa katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar wakati wa mkutano na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi alipokuwa na mazungumzo na Ujumbe wa Taasisi ya ULINGO na kukabidhiwa TUZO Maalum ya pongezi kwa utendaji wake wa kazi.
WAJUMBE wa Taasisi ya Tanzania Women Cross Party Platform (ULINGO) wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza wakati wa mkutano wao uliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 12-6-2023, walipofika Ikulu kwa ajili ya kumkabidhi TUZO maalum ya kumpongeza
WAJUMBE wa Taasisi ya Tanzania Women Cross Party Platform (ULINGO) wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza wakati wa mkutano wao uliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 12-6-2023, walipofika Ikulu kwa ajili ya kumkabidhi TUZO maalum ya kumpongeza

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.