Habari za Punde

Rais Dk Hussein Mwinyi akutana na msanii maarufu wa sanaa yua filamu kutoka China Ikulu

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi wakisalimiana na mgeni wao Msanii Maarufu wa Sanaa ya Filamu  kutoka Nchini China Mr.Jin Dong, alipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu 10-8-2023.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika mazungumzo na mgeni wake Msanii Maarufu wa Sanaa ya Filamu kutoka Nchini China Mr. Jin Dong, alipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar leo 10-8-2023 na (kushoto kwa Rais) Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikabidhi zawadi ya Mlango wa Zanzibar mgeni wake Msanii Maarufu wa Sanaa ya Filamu kutoka Nchini China Mr.Jin Dong, baada ya kumaliza mazungumzo yake yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar leo 10-8-2023, na (kushoto kwa Rais) Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi.(Picha na Ikulu)
MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi akimkabidhi zawadi ya Sanduku la Kasha Msanii Maarufu wa Sanaa ya Filamu kutoka Nchini China Mr.Jin Dong, baada ya kumaliza mazungumzo yake na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 10-8-2023.(Picha na Ikulu)

 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi, wakiagana na mgeni wao Msanii Maarufu wa Sanaa ya Filamu kutoka Nchini China.Mr.Jin Dong, baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 10-8-2023.(Picha na Ikulu) 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema ujio wa nyota maarufu wa filamu nchini China, Jin Dong, utaendelea kuifungulia Zanzibar soko la Utalii kutoka China.

Dk. Mwinyi ameyasema hayo Ikulu, Zanzibar alipotembelewa na msanii huyo ambaye yupo Zanzibar kwa kazi ya kutengeneza filamu.

Alisema, ujio wake ni fursa adhimu kwa Zanzibar kutangazwa kimataifa hasa kupitia Sekta ya Utalii ambayo ni Sekta mama ya uchumi wa Taifa.

Rais Dk. Mwinyi alimueleza mgeni wake huyo, kwamba Zanzibar ina vivutio vingi vya Utalii, ukiwemo Utalii wa fukwe safi nyeupe zinazovutia wengi duniani, Utalii wa utamaduni, Utalii wa Mji mkongwe, Utalii wa michezo, Utalii wa visiwa pamoja na wa Mikutano.

Aidha, alimkaribisha mgeni huyo kuitumia fursa ya kuwepo kwake Zanzibar kutembelea maeneo muhimu ya Utalii likiwemo shamba la viungo vya Zanzibar, Kisiwa cha Mnemba, Kaskazini Unguja pamoja na Mji Mkongwe wa Zanzibar.

Naye, nyota huyo wa Filamu nchini China, Jin Dong, alimueleza Rais Dk. Mwinyi furaha yake ya kufika Afrika kwa mara ya kwanza tena ndani ya visiwa vya Zanzibar kwa nchi za Afrika Mashariki.

Alisema, mbali na Safari ya Sanaa hapa Zanzibar lakini pia ujio wake unaimarisha uhusiano wa undugu na urafiki uliopo baina ya China na Tanzania ikiwemo Zanzibar.

Aliahidi kuwa balozi mzuri wa kuitangaza Zanzibar kwa Utalii na alieleza imani yake ya kuwavutia Wachina wengi kuja kutalii visiwa vya Zanzibar.

Miongoni mwa maeneo ya Utalii aliyotembezwa msanii huyo ni kisiwa cha Mnemba, Mji Mkongwe maeneo ya Forodhani na Ngome Kongwe.

Jin Dong ni nyota mkubwa China mwenye wafuasi wa mitandao ya kijamii zaidi ya milioni 15. Mbali na kazi za Sanaa pia ni Mwanasiasa nai Naibu Mkurugenzi wa kikundi cha Sanaa cha serikali cha utamaduni.

IDARA YA MAWASILIANO IKULU, ZANZIBAR

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.