MLEZI
wa Jumuiya ya CCM ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Mke wa Rais wa Zanzibar,
Mama Mariam Mariam ameipongeza jumuiya hiyo kwa kuwa na viongozi imara wenye
dira ya maemdeleo endelevu na mioyo ya kujituma kuwapambania wanawake wa
Tanzania na vijana.
Mama
Mariam Mwinyi alitoa pongezi hizo alipozungumza na uongozi wa UWT ukiongozwa na
Katibu mkuu wake, Jokate Mwegelo na ujumbe wake waliofika Ikulu ya Migombani, Mkoa
wa Mjini Magharibi.
Mama
Mariam Mwinyi ambae pia ni Msarifu na Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini ya Taasisi
ya “Zanzibar Maisha Bora Foundation” (ZMBF), aliueleza uongozi huo kuhusu taasisi ya (ZMBF) inavyounga mkono juhudi za
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Sera yake ya Uchumi wa Buluu
unaoshajihisha wananchi zaidi kuzitumia fursa za bahari kuleta maendeleo ya
kiuchumi na kujiongezea kipato kupitia kilimo cha mwani.
Alisema,
taasisi ya ZMBF imewawezesha kiuchumi
wanawake na vijana hasa wakulima wa mwani baada ya kuwaweka pamoja kinamama wa
Unguja na Pemba kwa lengo la kuwapa mikopo nafuu ili kuendeleza zao hilo
linaloongoza kulimwa Zanzibar na kuwa nchi ya kwanza Afrika na ya pili kwa
dunia nzima ikiongozwa na Ufilipino.
Alisema, kilimo cha mwani
Zanzibar kinakamata asilimia tatu ya pato la taifa baada ya Utalii unaochangia
asilimia 30 ya pato la taifa na kilimo cha Karafuu.
Alisema.
mbali na fursa nyingi zinazotokana na zao la mwani ikiwemo kutumika kama,
chakula, dawa, vipodozi, virutibisho vya mwili na kuongeza lishe mwilini pia zao
hilo linaimarisha sana afya za mama wajawazito.
Mbali na shughuli nyingi
zinazofanywa na taasisi ya ZMBF ikiwemo udhalilishaji masuala ya wanawake,
vijana na watoto pia kuendeleza Kampeni yake ya “Mariam Mwinyi
Walkathon” ambayo imewagusa wananchi wengi na kuwafuata walipo ili uchunguza
afya zao na kufanya matibabu, Mama Mariam Mwinyi aliwaeleza UWT kwamba lengo la
kampeni hiyo ni utekelezaji wa mikakati ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwafikishia
huduma bora za matibabu wananchi wake.
Pia
Mama Mariam Mwinyi alimpongeza Katibu Mkuu Jokate Mwegelo kwa kuteuliwa kushika
nafasi hiyo hivi karibuni na kukipongeza chama cha CCM kwa kufanya uteuzi
sahihi.
Vile
vile, Mama Mariam Mwinyi alipongeza
hatua ya UWT kupongeza juhudi za miaka mitatu ya uongozi wa Rais D.k. Hussein
Ali Mwinyi nakueleza wanafanya uamuzi sahihi.
Naye,
Katibu Mkuu huyo wa Umoja wa Wanawake Tanzania, Jokate Mwegelo alipongeza hatua
ya Mama Mariam Mwinyi kujikurubisha kwa wananchi na kushirikiana nao kwenye masuala
mbalimbali ya maendeleo ikiwemo kuishajihisha jamii kufanya mazoezi kwa
kuungana nao pamoja na kuimarisha afya zao ili kuepukana na maradhi mbalimbali
ya kuambukiza na yasiyoyakuambukiza.
Alisema,
UWT inabeba agenda zote zinzazowahusu wananwake bila kujali tofauti zao
kisiasa, dini, ukabila, rangi wala kipato na uchumi wao.
Katibu
Joketi pia alipongeza mabadiliko ya maendeleo yanayofanywa na Rais Dk. Mwinyi
kwa kipindi kifupi Zanzibar imekua na maendeleo makubwa na kusifu jitihada za
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar hasa kwenye suala zima la kuimarisha
miundombinu ya barabara na mawasiliano na huduma za jamii ikiwemo afya, maji
safi na elimu.
Kamati
kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, hivi karibuni ilimteua Katibu Mkuu Jokate
Mwegelo kushika wadhifa huo, awali aliwahi kushika nafasi mbalimbali za chama
na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwemo Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe,
Pwani, Temeke na Korogwe Mkoani Tanga.
IDARA YA MAWASILIANO,
IKULU ZANZIBAR
No comments:
Post a Comment