Mhe. Hemed amezitaka kampuni ya Lancet na Saifee amabazo zimepewa mkataba wa kutoa huduma hospitalini hapo kuhakikisha huduma zote zinapatikana kwa wakati na kwa ubora wa hali ya juu kama makubaliano yanavyoelekeza.
Sambamba na hayo amewataka wahudumu na madaktari kuendelea kutumia lugha nzuri na kufuata maadili yao ya kazi wakati wanapowahudumia wagonjwa wanaofika kupatiwa huduma hospitalini hapo pamoja na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa madaktari na wahudumu sambamba na kuilinda miundombinu iliyomo hospitalini ili iweze kudumu na kutumika kwa muda mrefu.
Nae Waziri wa Afya Mhe Nassor Ahmed Mazurui amesema hudu za Afya zimeimarika zaidi Zanzibar ndani ya miaka mitatu (3) ya Uongozi wa Rais Dk Mwinyi kwa kujengwa mahospitali ya Wilaya, Mkoa na zile za Rufaa pamoja na kufanyiwa maboresho makubwa baadhi ya vituo vya Afya.
Amesema kuwa hospitali na vituo vya Afya vilivyojengwa vimekidhi viwango na ubora, pamoja na kuwepo vifaa tiba vya kutosha kulingana na uhitaji sambamba na utolewaji wa huduma za matibabu kwa wananchi wote bila ya ubaguzi na kufikia zile fikra na mawazo ya waasisi wa mapinduzi akiwemo rais wa kwanza wa Zanzibar Marehemu Sheikh ABEID AMANI KARUME.
Akitoa Taarifa ya Kitaalamu kuhusu ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kati ya Mwera Ponge Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Amour Suleiman amesema Jumla ya shilingi Bilioni 9.7 zimetumika katika Ujenzi wa Mradi wa Hospital hiyo ambapo kwa wakati mmoja ina uwezo wa kulaza zaidi ya wagonjwa mia moja(100) na kupatiwa matibabu hospitalini hapo.
Amesema kuwa hospitali hiyo ya Wilaya inatoa huduma mbali mbali ikiwemo Huduma ya mama na mtoto, huduma ya maabara, huduma ya magojwa ya dharura hivyo amewataka wananchi kuendelea kuitumia vizuri hospitali hiyo kwa kutoa ushirikiano kwa madaktari na watoa huduma hospitalini hapo ili kuweza kufikia malengo ya mapinduzi matukufu ya mwaka 1964 ya kutoa huduma bora kwa kila mwnanchi.
Imetolewa na kitengo cha Habari (OMPR)
tarehe 02.01.2024
No comments:
Post a Comment