Waziri
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo
akishiriki Mkutano wa Sita wa Baraza la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEA6) unaofanyika
katika Makao Makuu ya Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP) jijini
Nairobi, Kenya ambapo ulifunguliwa Februari 26, 2024 na kutarajiwa kuhitimishwa
Machi 01, 2024.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo
anashiriki Mkutano wa Sita wa Baraza la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEA6) unaofanyika
katika Makao Makuu ya Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP) jijini
Nairobi, Kenya.
Kupitia mkutano huo viongozi kutoka mataifa mbalimbali duniani ikiwemo Tanzania wanajadili namna ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi, uharibifu wa baionuayi na uchafunzi wa mazingira.
Kama inavyofahamika Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazokabiliwa na athari za mabadiliko ya tabianchi ambayo husababisha ukame, uhaba wa mvua, mafuriko na vifo vya mifugo.
Pamoja na kushiriki Mkutano wa UNEA6, katika kukabiliana na changamoto hizo Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali kuhakikisha taifa linakuwa salama.
Lengo la mkutano huo ni kuunda sera kuhusu mazingira ambapo UNEA linalenga kurejesha maelewano kati ya binadamu na mazingira na hivyo kuboresha maisha ya watu wanaokabiliwa na changamoto za mazingira.
Hivyo, mkutano huu ni fursa pia kwa serikali za nchi 193
wanachama wa Umoja wa Mataifa, wanaharakati wa mazingira, wanasayansi na sekta
binafsi kupaza sauti na kuhusishwa katika kutunga sera ya ulimwengu mzima
kuhusu mazingira.
Ujumbe wa Tanzania umeambatana na Waziri
Dkt. Jafo ni Naibu Katibu Mkuu (Muungano) Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Abdallah
Hassan Mitawi na wataalamu kutoka Ofisi hiyo.
Mkutano
huu wenye kaulimbiu ‘Juhudi madhubuti, jumuishi na endelevu za kukabiliana na
mabadiliko ya tabianchi, uharibifu wa bayoanuai na uchafuzi‘ ulifunguliwa unatarajiwa
kuhitimishwa Machi 01, 2024.
No comments:
Post a Comment