Meza kuu wakiongoza Mkutano 33 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango ngazi ya Wataalam unaofanyika jijini Arusha
Mkutano 33 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri linaloshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mipango umeanza leo tarehe 3 Juni 2024 jijini Arusha.
Mkutano huo wa siku tano kuanzia Juni 3-7, 2024 umeanza kwa Ngazi ya Wataalam na na baadaye utafuatiwa na Ngazi ya Makatibu Wakuu utakaofanyika tarehe 6 Juni 2024 na kuhitimishwa na Mkutano Ngazi ya Mawaziri ukaofanyika tarehe 7 Juni 2024.
Mkutano huo katika Ngazi ya Wataalam pamoja na mambo mengine utapokea na kujadili mapendekezo na taarifa mbalimbali za Jumuiya ikiwemo: Utekelezaji wa Itifaki ya Soko la Pamoja la Jumuiya; Mapendekezo ya kuhuisha Mipango ya Jumuiya na Mipango ya Nchi Wanachama; Taarifa ya Wakurugenzi wa Masuala ya Kazi kuhusu Ukamilishaji wa Rasimu Iliyorekebishwa ya Sera ya Uhamiaji ya Wafanyakazi wa Jumuiya.
Masuala mengine yatakayo jadiliwa ni pamoja na taratibu za Uanzishwaji wa Jukwaa la Mashauriano kuhusu Uhamaji katika Jumuiya ya Afrika Mashariki; Kuidhinisha Sera na Mkakati wa Pili wa Mawasiliano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki; na Kuidhinisha Kalenda ya Shughuli za Jumuiya kwa kipindi cha Julai – Desemba 2024.
Akifungua mkutano huo Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya
Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya forodha, biashara
na fedha Bi. Annette Ssemuwemba amehimiza kuhusu
umuhimu wa mkutano huo katika kusimamia utekelezaji na
ufanisi wa sera na mipango ya Jumuiya ili kukidhi matarajio
ya Wananchi.
“Mtakumbuka kuwa takriban miaka miwili sasa hakupata
fursa ya kufanya mkutano huu, kwa sababu hiyo kwa umoja
wetu tutumie fura hii hadhimu kujadili na kutafuta
majawabu yatakayotupa uelekeo mpya na sahihi wa
kutekeleza na kusimamia kwa ufanisi sekta mbalimbali
ikiwemo bishara na fedha kwa maendeleo ya Jumuiya
yetu” Alieleza Bi. Annette Ssemuwemba.
No comments:
Post a Comment