Habari za Punde

Viongozi wa Dini na Wanasiasa kuwahubiria Amani waumini na wafuasi wao ili nchi iendelee kuwa na Utulivu

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na kuwasalimia Waumini wa Dini ya Kiislam, baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa, iliyofanyika leo 6-12-2024 katika Masjid Shaafiy Mbuyu Mnene Wilaya ya Magharibi “B” Unguja.


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na kuagana na Viongozi wa Masjid Shaafiy Mbuyu Mnene Wilaya ya Magharibi “B” Unguja, baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa iliyofanyika leo 6-12-2024 katika Masjid hiyo.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi  ameisistiza jamii kuendelea kuitunza Amani iliopo  wakati nchi ikielekea kwenye mwaka wa Uchaguzi Mkuu. 

Alhaji Dk. Mwinyi ametoa tamko hilo alipozungumza na Waumini wa dini ya Kiislamu wa kwenye ibada ya sala ya Ijumaa, Masjid Shaafy uliopo Mombasa Mbuyu Mnene, Wilaya ya Magharibi  B.

Ameeleza  ni wajibu wa Viongozi wa Dini na Wanasiasa  kuwahubiria Amani  waumini  na wafuasi  wao  ili nchi iendelee  kuwa na Utulivu na Serikali iendelee na mipango ya Maendeleo.

Alhaji Dk. Mwinyi amefahamisha  kwa miaka minne  nchi imekuwa  na  utulivu mkubwa  wa kupigiwa mfano  hali inayohitaji kuendelezwa  kuelekea Uchaguzi Mkuu  wa 2025.

Ameeleza  kuwa kwa miaka mingi iliopita Uchaguzi  ulikuwa ni sababu ya nchi kuingia katika mifarakano  isio na tija kwa Nchi.

Amesisitiza  ni vyema kila mwananchi kuwa  na  dhamira ya dhati ya  kuimarisha Amani  ili nchi isiingie  katika Uhasama na kutokuelewana.

Khatibu wa  Masjid Shaafy Khamis  Shaaban   amewakumbusha  Waumini wa Dini ya Kiislamu  kuwa na Subira na  Ustahamilivu  pamoja na kumcha Mwenyezi Mungu  kila Wanapopatwa na mitihani ya Kidunia.

Ameeleza kuwa dunia ina mitihani  na majaribu mengi  na kuwahimiza kumrudia Mungu kwa  Sala na Kumshukuru ili kupata shufaa.

Kwanupande wake Katibu wa Afisi ya Mufti, Sheikh Khalid  Ali Mfaume  amewanasihi Waumini hao kufahamu kuwa Dunia ni pahala  pa  kutenda mambo mema  na kuwa na subira kwani malipo ya wanaosubiri ni pepo. 

Wakati huo huo Alhaj Dk,Hussein Ali Mwinyi alifika Hospitali ya  Rufaa  ya  Mkoa  Lumumba  kuwafariji na kuwajulia hali Wagonjwa waliolazwa Hospitalini hapo akiwemo  Mzee wa Chama cha Mapinduzi  Haji Machano .

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.