Habari za Punde

Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar Mhe. Jaji Aziza Iddi Atembelea Vituo vya Uandikishaji Vituo vya Wapiga Kura Wilaya ya Magharibu "A" Umguja

Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar Jaji Aziza Idi Suwedi akizungumza na Mawakala wa Vyama vya Siasa  wakati alipotembelea Vituo mbalimbali vya Wilaya ya Magharibi A na Kutatua Changamoto zilizojitokeza  Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.

Na Rahma Khamis Maelezo  Zanzibar.

Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Jaji Aziza Idd Suwed amewataka wananchi wa Wilaya ya  Magharibi ‘B’ waliotimiza vigezo kujitokeza kuandikisha katika daftari la wapiga kura awamu ya ya pili linalotarajiwa kuanza kesho Mach 4 ili kupata haki ya kupiga kura.

 

Wito huo ameutoa skuli ya Regeza Mwendo Mwera Wilaya ya Magharibi A, wakati akitembelea vituo vya kuandikisha wapiga kura Wilayani humo ikiwa ni muendelezo wa ziara zake za kutembelea vituo vya uandikishaji wa daftari la wapiga kura.

 

Amesema kuwa Tume ya Uchaguzi inaendelea na zoezi la kutembelea vituo hivyo kwa lengo la kuangalia hali ya uandikishaji inavyendelea pamoja na kuangalia changamoto zilizopo ili kuwaondoshea usumbufu wananchi .

 

Aidha  ameeleza kuwa wananchi wamehamasika kujitokeza kujiandikisha katika daftari hilo na bado wanaendelea kuwasisitiza wapiga kura katika Wilaya zilizobakia kufika kwa wingi kwenye vituo vya uandikishaji ili kupata haki yao ya msingi.

 

Nao Mawakala na Wakuu wa Vituo vya kuandikisha wamesema kuwa vituo vipo katika hali ya usalama hakuna tatizo lolote na wananchi wanaendelea kujitokeza na kujiandikisha katika daftari la wapiga kura.

 

  Kwa upande wao wananchi waliyojiandikisha katika daftari hilo wamesifu utaratibu unaotumika na zoezi linaendelea vizuri hakuna matatizo kila mwenye sifa ya kuandikishwa anapata fursa hiyo na zoezi hilo linatarajiwa kukamiliika leo Wilayani humo.

Wakala wa Uandikishaji Wapiga Kura wapya Asma Waziri Mohamed akimsaidia Mwananchi salliekuja Kujiandikisha katika Shehia ya Kianga Wilaya ya Magharibi A katika Zoezi linaloendelea Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.
Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar Jaji Aziza Idi Suwedi akiwa pamoja na Makamishna wa Tume ya Uchaguzi  wakitembelea moja katika Vituo  vya Uandikishaji wapiga kura wapya Shehia ya Mwera Wilaya ya Magharibi A Unguja na Kutatua Changamoto zilizojitokeza.

Sheha wa Shehia ya Muembemchomeke  Ali Haji Nemshi akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusiana na Zoezi la Uandikishaji wapiga Kura linaloendelea katika Shehia hio,Wilaya ya Magharibi A Unguja.
Picha na Yussuf  Simai - Maelezo Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.