Mwajuma Mmanga
na Kauthar Abdalla
WAZIRI wa Habari
Utamaduni Utalii na Michezo, Said Ali Mbarouk amesema Zanzibar ina historia ya
kipekee kwenye tasnia ya habari katika bara la Afrika na kuliomba Baraza la
Habari Tanzania (MCT), kusaidia wataalamu watakaoiandika historia hiyo.
Waziri huyo
alieleza hayo katika ukumbi wa Zanzibar Beach Resort kwenye kongamano
lililofuatiwa na mkutano mkuu wa mwaka wa Baraza la Habari Tanzania (MCT).
Alisema wakati
umefika wa historia ya vyombo vya habari Zanzibar kuandikwa kitaalamu hali
itakayosaidia vizazi vijavyo kuifahamu vyema na kuwa kama muongozo wa
kuendeleza mazuri waliyoasisiwa.
‘Naiomba sana
MCT, itumie wataalamu wasaidie kuaindika upya historia ya vyombo vya habari ya
Zanzibar’, alisema waziri huyo.
Aidha waziri
huyo aliwataka waandishi wa habari Tanzania kuhakikisha wanafuata maadili kwani
ndiyo nguzo muhimu ya kuipeleka mbele kada hiyo yenye umuhimu mkubwa katika
kukuza maendeleo.
Awali
akiwasilisha mada katika kongamano hilo, Muhadhiri Muandamizi Ayub Rioba,
alivitaka vyombo vya habari visilichukulie kwa mzaha suala la marekebisho ya
katiba mpya.
Alisema mchakato
wa mabadiliko ya katiba mpya ya Tanzania ni jambo lenye kuhitaji kuchukuliwa
kwa umakini na vyombo vya habari kwani ndilo litakaloweza kuijenga Tanzania
ijayo inayohitajiwa na vizazi vijavyo.
Aliwataka
waandishi wa habari waichambue kuitafsiri katiba jambo ambalo litawasaidia
wananchi sio kuifahamu tu bali pia litawawezesha kutoa maoni yenye mantiki.
Naye Timothy
Kitundu akieleza hali ya ajira kwa vyombo vya habari, alisema waandishi wa
habari wamekuwa mafundi wa kueleza dhiki za kiajira kwa taasisi nyengine huku
wao wenyewe pia wakikabiliwa na matatizo ya aina hiyo hiyo.
Alishauri uwepo
umoja ambao utawaunganisha wanahabari katika kutetea haki zao za msingi na
kuwafanya kupata maslahi kama wanavyonufaika wafanyakazi wa kada nyengine.
Wakichangia
katika kongamano hilo, Rose Mwalongo alisema limekuwepo tishio la kimaisha kwa
waandishi wenye kuandika habari za kiuchunguzi kutokana na kugusa malahi ya
watu wachache.
Naye Prof. Ruth
Meyena aliwataka waandishi wa habari waache kulalamika na badala yake wakae
pamoja kutafuta njia ambazo zitahakikisha wanaondokana na matizo waliyonayo.
Kongamano hilo
lililoandaliwa na MCT liliwashirikisha waandishi wa habari za ya 150 kutoka
Tanzania bara na Zanzibar.
0 Comments