Na Thompson
Mpanji, MBEYA
SERIKALI
mkaoni Mbeya imelimaliza sakata la mgomo wa Madaktari kwa aina yake baada ya
kupitisha maamuzi magumu ya kuwatimua kazi madaktari zaidi ya 72 wa mafunzo ya
vitendo walioajiriwa na hospitali ya Rufaa mkoani humo.
Akizungumza
na waandishi wa habari, Kaimu Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Dk.Norman Sigalla kwa
niaba ya Mwenyekiti wa bodi ya hospitali hiyo Abbas Kandoro, alisema bodi
imefikia kuchukuwa uamuzi mgumu
kutokana na madaktari kutotekeleza wajibu wao wa kuwahudumia wagonjwa.
Alisema
sababu nyingine ya kuchukuwa uamuzi huo madaktari hao hawakufika kazini na kukaidi ombi
la Mwenyekiti wa bodi kukutana nao kuwasikiliza sababu za kutofika kazini na
kujadili namna ya kumaliza matatizo yao.
Alifahamisha
kuwa kutokana na maamuzi hayo madaktari hao waliotimiliwa wametakiwa kuondoka
katika majengo ya hospitali waliyokuwa wanaishi.
Dk.Sigalla
alisema Juni 23 mwaka huu jumla ya madaktari 15 waliokuwa zamu
wakiwemo wa mafunzo 12 na walioajiriwa watatu hawakufika kazini, Juni 24
madaktari 19 wakiwemo wa mafunzo 15 na ‘registrars’ wanne hawakufika
kazini na kuanzia Juni 25 hadi jana imethibitika madaktari wa mafunzo
54 na walioajiriwa 18 hawajafika kazini.
Alifafanua
kuwa Bodi iliamua madaktari wote ambao hawafiki kazini waandikiwe barua za
kujieleza kwa nini wasichukuliwe hatua za kinidhamu kwa kuvunja mkataba
walioingia na hospitali na pia kukiuka kanuni za kudumu za utumishi wa
umma toleo la 2009 kif.f.16-f.17 na F.27.
Kaimu
Mkuu huyo wa Mkoa alisema hadi kufikia jana siku zilizotolewa na bodi zilikuwa
zimemalizika na hivyo wamewaandikia barua za kusitisha ‘internship’
katika hospitali ya Rufaa Mbeya na kuwarudisha kwa Katibu Mkuu na kuwataka
wanaokaa hosteli waondoke kabla ya saa 11.00 za jioni leo.
Alisema
madaktari 18 walioajiriwa wanakabidhiwa barua zao za kusimamishwa
ajira yao katika hospitali ya Rufaa Mbeya na kurudishwa
wizarani kwa Katibu Mkuu kwa hatua stahiki za kinidhamu na kutakiwa
kukabidhi mali za ofisi.
Dk.Sigalla
alikiri kuongezeka kwa mzigo lakini hawajatetereka,bodi
iliwasiliana na Taasisi mbalimbali Mbeya na nje ya mkoa ili kupata
wafanyakazi wa kusaidia kupunguza makali ya upungufu wa wafanyakazi na
wamepata ushirikiano kutoka kwa Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya kwa
kupatiwa madaktari watano kusaidia.
Akizungumzia
hali ilivyo kwa sasa Mkurugenzi wa hospitali ya Rufaa Mbeya, Dk.Eliuter Samky
alisema licha ya kuongezeka kwa mzigo lakini wanatarajia madaktari
wataalamu (specialist) 22 waliobaki na na walioajiriwa 13
watafanyakazi za kutoa huduma bila wasi wasi.
Awali
gazeti hili limeshuhudia baadhi ya madaktari katika hosteli wakiwa katika
pilika za kupakia mizigo katika gari ndogo ya kukodi ya
abiria taksi na kuondoka katika eneo la hospitali ya Rufaa huku wakiwa
hawataki kupigwa picha wala kuhojiwa.
Juni,
22 mwaka huu Mahakama kuu ya kazi Tanzania kanda ya Dar es
Salaam chini ya jaji S.C.Moshi ilitoa natisi ya kuzuia mgomo wa madakatari.
0 Comments