SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar,
imesema itaangalia uwezekano wa kukaa pamoja na wizara ya Makamu wa Kwanza wa Rais kuona namna watavyoweza kumpatia msaada
mtoto mwenye ulemavu aliyebakwa na kupewa ujauzito.
Waziri wa Ustawi wa Jamii, Maendeleo ya
Wanawake na Watoto, Zainab Mohammed Omar, aliyasema hayo jana katika kikao cha
Baraza la Wawakilishi kinachoendelea mjini Zanzibar, wakati akijibu suala la Mwakilishi
wa Nafasi za Wanawake Wanu Hafidh Ameir.
Mwakilishi huyo alitaka kujua serikali ina
mpango gani wa kumsaidia mtoto huyo kwa kushirikiana na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais kwa vile mtoto huyo hana uwezo wa kumtunza
mtoto huyo.
Akijibu suala hilo, waziri huyo alisema ni
kweli serikali imeliona hilo tatizo na itafikiria kukaa pamoja na wizara ya Makamu
wa Kwanza wa Rais baada mtoto kuonekana uwezo wake ni mdogo wa kujitunza huku
akiwa ni mlemavu.
Alisema wataliangalia hilo ili kuona mtoto huyo anapata misaada
itayoweza kumsaidia kukimu maisha yake kwani hivi sasa yupo katika hali
itayoweza kumpa mzigo kuendesha maisha yake.
Akijibu suala la nyongeza la Asha Bakari
Makame, aliyehoji kama ina mpango wa kukata rufaa kwa vile inaonekana katika
suala la mtoto huyo kudaiwa na vyombo vya sheria kukosa ushahidi juu ya suala
hilo na huenda kukawa na uzembe wa makusudi unaofanywa na taasisi hiyo.
Waziri huyo alisema wizara hiyo mara zote
imekuwa na utaratibu wa kukata rufaa juu ya matukio ambayo huyaona ipo haj ya
kufanya hivyo.
Akiendelea kujibu suala la Mwakilishi wa
Wanawake Amina Iddi Mambrouk, aliyetaka kujua ni lini kipimo cha DNA kitaweza
kupatikana.
Akijibu suala hilo Waziri huyo alisema serikali bado
inahangaika kupata kipimo cha DNA, na ni vyema wananchi wakasubiri kufanikishwa
kwa mpango huo.
Kuhusu suala la Msingi la Mwakili wa Wnawake
Mgeni Hassan Juma, aliyetaka kufahamu kama Wizara hiyo inafahamu taarifa za
kubakwa kwa mtoto huyo baada ya kuripotiwa katika Gazeti la Zanzibar Leo,
alisema Wizara hiyo ilifuatilia suala hilo
katika kituo cha mkono kwa mkono pamoja na Polisi Mazizini na mtuhumiwa tayari
amechukuliwa vipimo vya D.N.A.
Alisema kutokana na taratibu za kisheria suala
hilo bado lipo
katika kituo cha Polisi cha Mazizini ikiwa inasubiri kupatikana kwa
ushahidi wa kipimo cha D.N.A ili kuweza
kuifikisha Mahakamani kesi hiyo.
Alisema ingawa Wizara hiyo imekuwa ikichukua
hatua mbali mbali za kukabiliana na tatizo hilo lakini bado kuna mambo ambayo
yameonekana kukwaza jitihada hizo likiwemo suala la ushirikiano mdogo kwa jamii
katika suala zima la kutoa ushahidi Mahakamani, upelelezi wa Polisi kuchukua
muda mrefu kutokana na ushirikiano na jamii na hukumu kuchelewa.
0 Comments