6/recent/ticker-posts

Al Madrasatul Lailahailallah Imeanda Mashindano ya Kuhifadh Quran.

Na Maryam Kidko/Salma Nassor- Maelezo Zanzibar.

Viongozi wa Chuo cha Almadrasatul –Lailahailallah iliopo kitope Wilaya ya Kaskazini B  imeandaa mashindano  ya kuhifadhi qur-ani kwa akina mama watu wazima .

Mashindano hayo yaliyofanyika  leo  katika Uwanja wa Mpira wa Kombora Kitope Mkarakatini yalijumuisha akinamama kutoka Vyuo vya Wilaya ya Kaskazini A na Kaskazini B pamoja na Mkoa wa Mjini Maghrib.

Mwalimu Mkuu  Ustaadh Omar Saidi Moh’d kutoka Almadrasatul- Lailahailallah amesema lengo kuu la madrasa  kuandaa mashindao hayo ni kuwashajihisha Wazee kujua umuhimu wa elimu  ili na wao waweza kuwasimamia watoto wao kuepukana na vitendo viovu.

Amesema kuwa elimu ya dini ya kiislamu  inamgusa kila muislam  mkubwa na mdogo hivyo ipo haja  kwa waislamu kujitokeza  kuitafuta elimu na kusoma Qur-ani kwani ni kitabu kitakatifu kwa waislamu wote.

Mlezi wa Almadrsatul-lailahailallah Khamis Ndende Juma amesema Chuo hicho kimeshashiriki katika mashindanio mbalimbali yakiwemo ya Mkoa na Wilaya na imeweza kufanya vizuri katika mashindano hayo.

Hata hivyo amewashauri wanaume kujenga tabia ya kuwaruhusu wake zao kushiriki katika madras mbali mbali  ili waweze kupata elmu  na maadili ya kiislamu, 

Akitaja baadhi ya Changamoto zinazoikabili Madrasa hiyo  amesema ni ukosefu wa Vyoo pamoja na uhaba wa nafasi ya kusomea Wanafunzi  na kuwataka watu wenye uwezo kusaidia  ili waweze kupokea wanafunzi wengi zaidi.

Jumla ya Vyuo 9 vimeshiriki katika mashindano hayo yaliyo jumuisha juzuu moja hadi juzuu ya nane.                                   
                                                  MWISHO
                          IMETOLEWA NA HABARI MAELEZO ZANZIBA.

Post a Comment

0 Comments