6/recent/ticker-posts

Kamati ya maafa yakutana Pemba kujadili kipindupindu Kojani

 MWENYEKITI wa kamati ya Mafaa Kisiwani Pemba, ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa kusini Pemba Mhe:Mwanajuma Majid Abdalla, akifungua kikao cha dharura cha kukabiliana na maafa juu ya hali ya Ugonjwa wa kipindupindu uliojitokeza katika Kisiwa Cha kojani, kikao hicho kilichohudhuriwa na maafisa wadhamini, wakuu wa Wilaya na makatibu Tawala huko katika ofisi ya Mkoa wa kusini Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 MAKATIBU Tawala kutoka Wilaya mbali mbali kisiwani Pemba, wakimsikiliza kwa makini Mwenyekiti wa kamati ya Maafa Kisiwani humo, ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa kusini Pemba Mhe:Mwanajuma Majid Abdalla, wakati alipokuwa akifungua kikao hicho kujadili hali ya Ugonjwa wa kipindupindu uliojitokeza katika kisiwa Cha Kojani.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 KATIBU Mkuu Wizara ya Afya Zanzibar Mhe:Saleh Mohammed Jidawi, akitoa taarifa ya hali ya Ugonjwa wa kipindupindu kwa Upande wa Unguja ulivyojitokeza na jinsi hatua zilivyochukuliwa, wakati wa kikao cha kamati ya Maafa Pemba ilipokutana.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
 AFISA Mdhamini Wizara ya Afya Pemba Dk Mkasha Hija Mkasha, akitoa taarifa ya hali ya kipindupindu ilivyo katika kisiwa cha Kojani, wakati kamati ya maafa Pemba ilivyokutana katika ofisi za Mkuu wa Mkoa wa kusini Pemba, juu ya kutathimi ya ugonjwa huo na mikakati ya kudhibiti usiendelee kutokea katika maeneo mengine.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)


  MRATIB wa Idara ya Maafa Kisiwani Pemba Khamis Arazak, akitoa taarifa ya uwepo wa vifaa mbali mbali vya kukabiliana na maafa wakati yatakapojitokeza, katika kikao cha kamati ya maafa Pemba ilipokutana.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
MKUU wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Mhe:Omar Khamis Othaman, akizungumza na wajumbe wa kamati ya mafia kisiwani Pemba, ilipokutana na kuonesha jinsi ya mikakati waliyoichukuwa katika mkoa wake katika kudhibiti Ugonjwa huo hauenei maeneo mengine.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

Post a Comment

0 Comments