Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar Dr Sada Mkuya Salum amewasilisha muelekeo wa Mpango wa maendeleo na Bajeti ya Serikali 2023/2024 na kueleza kwamba kutakua na mazingatio mahsusi ikiwemo ongezeko la Bajeti ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo, pensheni ya Wastaafu na Pensheni Jamii, kuanza kulipa asilimia 3.5 ya mshahara kwa ajili ya mfuko wa huduma ya Afya, Ununuzi wa Vitendea kazi ikiwemo magari na ujenzi wa ofisi za serikali pamoja na kutoa kipaombele katika malipo ya madeni ya Wazabuni, Wakandarasi na Watumishi wa Umma.
SERIKALI KUENDELEA KUWEKA MAZINGIRA SALAMA KWA WENYE VIWANDA NCHINI
-
*Serikali kuendelea kuweka mazingira salama kwa wenye Viwanda vinavyofanya
kazi na kutatua changamoto kwa wakati ili kuendelea kulinda ajira za
Watanz...
10 minutes ago
0 Comments