Katibu Mkuu Wizara ya Afya Zanzibar Dkt Fatma Mrisho amesema iwapo kutakuwa na usimamizi na ukaguzi kwa Wauguzi na Wakunga katika sehemu zao za kazi kutaondokana na malalamiko kwa wananchi wanaofika kupata huduma za afya. Hivyo ameutaka Uongozi wa Idara ya Uuguzi na Ukunga kusimamia na kufanya Ukaguzi wa mara kwa mara katika Mahospitali na Vituo vya Afya ili wafanyakazi waweze kutoa huduma zenye ubora.
0 Comments