6/recent/ticker-posts

WIZARA ya Afya Zanzibar imetitilina saini mkataba wa makubaliano na Taasisi ya Hodari kwa lengo la kuimarisha sekta ya afya

 Na.Wizara ya Afya Zanzibar 

WIZARA ya Afya Zanzibar imetitilina saini mkataba wa makubaliano na Taasisi ya Hodari kwa lengo la kuimarisha sekta ya afya kwenye upande wa kuwajengea uwezo wafanyakazi.

Akizungumza mara baada ya utiaji saini makubaliano hayo Katibu Mkuu Wizara ya Afya Zanzibar Dkt.Mngereza Mzee Miraji amesema kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imetoa kipaumbele cha kujifunza kwa watumishi wake ili kuendana na sayansi na Teknolojia.

Amesema Taasisi hiyo itahakikisha inatoa mafunzo ya mifumo ya kijidijitali ya afya hasa katika kufanya maamuzi ya haraka kwenye Sekta ya afya ikizingatiwa kuwa ni Taasisi ya mwanzo wazawa mbayo imekuja kushirikiana katika kufanya kazi katika sekta ya Afya.

Hata hivyo katibu mkuu amesema kuwa wizara ya afya itaendelea kushirikiana na wadau mbali mbali wa maendeleo katika kupeleka mbele sekta ya afya na ameipongeza taasisi hiyo kwa kuwa taasisi ya kwanza ya wazawa kutoa mafunzo ya digital health.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu na Mkufunzi wa Taasisi ya HODARI Dkt.Zeyana Abdallah Hamid amesema kuwa Taasisi hiyo itahakikisha inawajengea uwezo wafanyakazi wa Wizara ya Afya na Hospitali  katika kuimarisha Mifumo ya Taaria za afya kijidigitali.

Amesema mafunzo hayo watakayoyatoa yatawezesha kuimarisha matumizi ya taarifa za afya na mifumo, kupitia sera na mipango kazi ya Afya kurahisisha matumizi utoaji wa taarifa pamoja na kupanga mikakati kupitia taarifa zinazopatikana kwenye mifumo ya kijidigitali.

Amefahamisha kubwa la kushirikiana na Sekta ya Afya ni kukabiliana na changamoto wanazokabiliana nazo katika sekta ya Afya na kuwa na mifumo yenye ubora

Nae Mkuu wa Kitengo cha usimamizi wa Takwimu za Afya kutoka Wizara ya Afya Zanzibar Abuu Yussuf Ismail amesema Wizara ya Afya inampango mkakati wa kidijitali zinazohusiana  taarifa zinazotoka kwenye Hospitali za Wilaya na vituo vya Afya kuzichakata taarifa hizo na kuzifanyia maamuzi mbali mbali juu ya  taarifa hizo.

Amesema ushirikiano na Taasisi ya HODARI utaiwezesha Wizara ya  kupata wataalamu wazuri wa kuzichambua taarifa hizo ili kuzifanyia maamuzi sahihi taarifa hizo sambamba na kupanga mikakati itakayowezesha utoaji wa huduma kuwa wenye ubora zaidi.

Mratibu wa mifumo ya Taarifa Wizara ya Afya Zanzibar Fatma Khatib Haji amesema kuwepo kwa Taasisi hiyo kutawawezesha watendaji kupata ujuzi Zaidi na kuondokana na  changamoto ya  kutozitumia taarifa za afya zinazopatikana kupitia katika sehemu mbali mbali za Wizara hiyo.

Makubaliano baina ya Wizara ya Afya na Taasisi ya Hodari ni ya miaka mitatu ambapo lengo kubwa ni kuwapatia mafunzo  yatakayosaidia Serikali kupitia wizara ya afya kuzifatilia taarifa zinazopatikana kwenye mifumo ya kijidigitali ya wizara ya afya.

MWISHO

 

Post a Comment

0 Comments