6/recent/ticker-posts

Waziri Simbachawene kuliboresha Jeshi la Magereza

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene akikagua mazao katika shamba la mahindi linalomikiwa na Gereza la Kilimo na Mifugo la Kitengule ambapo jumla yae kari 160 zimelimwa zao hilo ambalo hutumika kwa ajili ya chakula cha wafungwa.Waziri Simbachawene yupo mkoani Kagera kwa ziara ya kikazi ya kukagua vyombo vya usalama vilivyopo chini ya wizara hiyo.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene akikagua mazao katika shamba la mahindi linalomikiwa na Gereza la Kilimo na Mifugo la Kitengule ambapo jumla yae kari 160 zimelimwa zao hilo ambalo hutumika kwa ajili ya chakula cha wafungwa.Waziri Simbachawene yupo mkoani Kagera kwa ziara ya kikazi ya kukagua vyombo vya usalama vilivyopo chini ya wizara hiyo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene akizungumza na Mkuu wa Magereza mkoa wa Kagera,Kamishna Msaidizi wa Magereza,Norbeth Komba(kulia) wakati wa ziara ya kutembelea shamba la mahindi linalomikiwa na Gereza la Kilimo na Mifugo la Kitengule ambapo jumla ya ekari 160 zimelimwa zao hilo ambalo hutumika kwa ajili ya chakula cha wafungwa.Waziri Simbachawene yupo mkoani Kagera kwa ziara ya kikazi ya kukagua vyombo vya usalama vilivyopo chini ya wizara hiyo.Kushoto ni Kamanda wa Polisi mkoa wa Bukoba

Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Na Mwandishi Wetu,KAGERA.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene ameweka wazi nia ya serikali kuunganisha nguvu kazi ya wafungwa na matumizi ya teknolojia katika kilimo ili Jeshi la Magereza liweze kuendana na kasi ya matumizi ya teknolojia ya kilimo hali itakayopelekea kuongezeka kwa uzalishaji huku akiweka wazi umuhimu wa kuijumuisha sekta binafsi katika shughuli mbalimbali za uzalishaji zinazofanyika katika maeneo ya magereza mbalimbali nchini.

Ametoa kauli hiyo leo, wakati wa ziara ya kukagua shughuli za Kilimo ikiwemo shamba la mahindi katika Gereza la Kilimo na Mifugo la Kitengule lililopo wilayani Karagwe mkoani Kagera akisisitiza kuwepo kwa ulazima na uharaka wa Jeshi la Magereza kubadili mtazamo ili na kuendana kasi na maendeleo ya sayansi na teknolojia katika kilimo ikiwemo matumizi ya mbegu bora na za kisasa na matumizi ya teknolojia.

‘Lazima twende kwenye mabadiliko,tutashirikiana na SHIMA(Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Magereza, tutahakikisha kwamba tunaingia kwenye kilimo ambacho tutatumia mashine kubwa ili tuweze kuzalisha kwa ukubwa na kimsingi tuna fursa ya kuilisha nchi nzima sio kuishia kulisha wafungwa tu,tuna maeneo makubwa tutashirikisha sekta binafsi kupitia SHIMA lakini pia tunataka Kwenda kwenye kilimo cha kidijitali kitakachofanya tutoke na tulime maeneo makubwa tuliyonayo kwa tija kubwa zaidi,nafahamu kuna jitihada zilianzishwa na wenzangu nataraji kuanzia walipoishia.’ Amesema Waziri Simbachawene.

Akizungumza wakati akisoma taarifa ya kilimo na mifugo, Mkuu wa Gereza hilo, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Mikael Mafwele ameweka wazi malengo yao sambamba na changamoto wanazokutana nazo ikiwemo upungufu wa mvua, wanyama waharibifu wa mazao ikiwemo nguruwe pori na nyani  ambao uharibu mazao.

‘Hapa tuna ekari 200 kwa ujumla wake lakini tumelima ekari 160 kumekuwepo na changamoto ya uchelewaji wa mvua ya kutosha hali inayopelekea kulima eneo dogo sambamba na kiwepo kwa Wanyama waharibifu wa mazao lakini tunaimarisha ulinzi ili kukabiliana na changamoto hiyo wa Wanyama wanaoharibu mazao.’ Amesema ACP Mafwele

Post a Comment

0 Comments