6/recent/ticker-posts

IGP WAMBURA AKAGUA MIRADI YA UJENZI MOSHI

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Camillus Wambura, akiwa 

ameambatana na Kamishna wa Fedha na Lojistiki CP 

Liberatus Sabas pamoja na maafisa wengine amefanya 

ukaguzi wa maendeleo ya Mradi wa Ujenzi wa nyumba za Wakufunzi na Familia zao na Mabweni ya Wanafunzi  katika shule ya Polisi Moshi Mkoani Kilimanjaro.

Ujenzi huo unatekelezwa na Serikali ya awamu ya sita chini  ya Amiri Jeshi Mkuu Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuwezesha na kuboresha upatikanaji wa miundombinu ya majenzi mbalimbali inayoendelea kutekelezwa ndani ya Jeshi la Polisi.

Itakapo kamilika miradi hiyo katika Shule hiyo ya Polisi Moshi utawaongezea morali katika utendaji kazi sambamba na kukuza ustawi wa askari kwa kukaa na kuishi kwenye mazingira bora na ya kisasa jambo litakalo wawezesha kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi.

Mbali na uboreshaji huo wa miundombinu ya makazi ya 

wakufunzi na wanafunzi  upo uboreshaji wa mitaala ambao 

umefanyika sambamba na kuingia kwenye mikataba na vyuo 

vya ndani ya nchi ili  kuendana na utekelezaji wa  

Mapendekezo ya Tume ya Haki Jinai iliyopendekeza Askari 

kujengewa uwezo ambapo imewezesha Maafisa, Wakaguzi na 

Askari 111 kufanikiwa kuhitimu masomo  katika kiwango cha 

Uzamili (Masters) kwa mwaka 2025 kutokana  na uwepo wa 

Tawi la IAA (Institute of Accountancy Arusha) katika Shule 

hiyo ya Polisi Moshi ambao wanaendesha kozi mbalimbali za 

kuwajengea uwezo na ujuzi Askari kwa kushirikiana na Jeshi 

la Polisi.







 

Post a Comment

0 Comments