
15.02.2026
Mkoa wa Mjini Magharib
Mwenyekiti
wa ACT Taifa Mhe. Othman Masoud , amesema kwamba bila uchaguzi huru na wa haki kwenye taifa lolote watu wote watakuwa ni watumwa ndani ya nchi yao kwa sababu haki ya kwanza ya wananchi ni
uwezo wa kuweka kiongozi unayemataka .
Mhe. Othman
ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar mstaafu ameyasema hayo
ukumbi wa Majid Kiembesamaki mkoa wa mjini Magharib alipozungumza na viongozi
wa chama hicho wa ngazi mbali mbali kutoka mikoa yote ya Unguja kutoa ufafanuzi
kuhusia na maendeleo ya mazungunzo ya kisiasa yanayoendelea.
Amesema
kwamba inapotokea mwananchi hana haki ya kuchagua na kuchaguliwa ni wazi kwamba
hakuna tofauti na kuwepo kwa ukoloni ndani ya taifa lao jambo ambalo halipaswi
kuwepo kwenye taifa lolote.
Aidha
amesema pia unapokosekana haki ya namna
hiyo katika taifa hilo hakutakuwa
na uwajibikaji na madaraka yanapotumika vibaya hakuna wakuchunguza kiongozi na
na kamwe taifa halitakuwa na mafanikio.
Mhe. Othman
amesema kwamba iwapo serikali na viongozi hawachungzwi kisheria na kikatiba
hakuna namna ya kuepuka wizi na ufisadi serikali na kuendelea kuwepo matumizi
mabaya ya madara ya umma kwa waliopo serikalini waliopewa dhamana ya kusimamia
mambo ya umma ndani ya taifa hilo.
Amesema
kwamba harakati za chama chake cha ACT kinapambania kuondosha mfumo na
utaratibu mbovu katika kusimamia na kuendesha nchi na pia kuondoa migogoro
ambayo kwa baadhi ya watu ni mtaji wa kujinufaisha binafsi na wanakuwa ni
wazito kuridhia inapotokea kuwepo
makubaliano pale penye mgogoro.
Hivyo ,
amesema kwamba hakuna nchi inayoweza kusonga mbele na ikawa na utulivu na amani ya kweli na
maendeleo thabiti kama nchi hiyo haina
katiba bora na pia viongozi waliopo wakailinda na kuifuata kikamilifu misingi ya katiba waliyonayo.
Amefahamisha
kwamba kuwepo mifumo bora na katiba yenye misingi madhubuti ndio inayosaidia kuwaweka wananchi pamoja na taifa likaweza kusonga mbele na kupata mafanikio ya kimaendeleo.
Mhe. Othman
aliyekuwa akifafanua hoja za mazungunzo ya kutafuta muafaka wakisiasa yanayoendelea,
amesisitiza kwamba msingi wa fitna iliyopo Zanzibar pamoja na mambo mengine ni
kukosekana katiba bora na kuwepo mfumo mbaya wa uchaguzi ambapo anatokea mtu
mmoja akamtangaza kiongozi kushinda uchaguzi pasipo na mamlaka ya kuhojiwa kwa
kuwa katiba inatoa mamlaka ya kifalme kwa waliopo madarakani.
Amesema
kwamba mazunguzo yanayoendelea ambayo yapo katika hatua kubwa ,chama chake
kinahitaji kuwepo makubaliano yataweza kusaidia kuijenga msingi imara ya
kikatiba Zanzibar , mfumo bora wa uchaguzi na kusimamia vyema haki za
kidemokrasia na uwajibikaji kwa manufaa ya Zanzibar.
Amesema
kwamba Zanzibar inahitaji kuwa na umoja wa kitaifa na maridhiano ya kweli kwa
manufaa ya taifa na kwamba si vyema nchi ikaendelea hivi inavyokwenda sasa na
kwamba ni vyema ikikubalika serikali ya pamoja isiwe ya paaa moja ikawanufaisha wachache kwa kupata
vyeo.
Pamoja na
hayo amesema kwamba ipo orodha ya mambo
12 muhimu ambayo yamejadiliwa ili na mengine yakikubalika yaweze kufanya
kazi vizuri katika kuchapuza kasi ya
kuleta mageuzi ya kweli Zanzibar, hata hivyo hakufafanua zaidi.
Naye Makamu
Mwenyekiti wa Chama hicho upande wa Zanzibar Ismali Jussu Ladhu, amewashukuru
wanachama wote wa chama hicho kwa
kuonesha na kufahamu dhamira ya kinachopambaniwa na chama hicho na kwamba
wamekuwa wakijitolea kufanya shughuli zote za chama kwa ari kubwa jambo ambalo
linakifanya chama hicho kuimarika licha ya misukosuko kinayopata.
Aidha amewataka
wanachama kufanya kazi kwa pamoja katika kutimiza yale yote yaliyodhamiwa na
kuweka malengo kuhakikisha kwamba chama kinatimiza azma yake ya kujenga na kumiliki ofisi na kumbi za mikutano
za kimataifa.
Naye
Mwenyekiti mstaafu wa chama hicho Babu Juma Duni Haji, amesema kwamba viongozi
wa Zanzibar kamwe hawapaswi kuyasahau malengo na dhamira ya mapinduzi ya mwaka
1964, kwamba ni ya kuondoa ubaguzi, mifarakano na dhulma za aina yoyote sambaba na kujenga maridhiano mingoni
mwa wananchi wa Zanzibar.
Kwa upande
wake Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Zanzibar Omar Ali Shehe, amesema kwamba Viongozi
wa chama hicho ngazi mbali mbali wameendelea kufanya kazi kila siku katika
kuhakikisha kwamba chama kinaaimarika na licha ya misukosuko ya uchaguzi,
lakini kimeendelea kuimarika kutokana na kazi kubwa ya kujenga chama
inayoendelea kufanyika.
Amesema
kwamba ahadi ya watendaji wa chama hicho ni kuhakikisha mbele ya mwenyekiti wa
taifa kwamba hatua yoyote itakayofikiwa
kwenye mazungunzo hayo wanachama wote wapo pamoja na viongozi na na kamwe
hawatorudi nyuma kwa kuwa wanapigania haki.
Mhe. Othman
amekamilisha vikao vyake na viongozi wa
chama hicho ngazi mbali mbali Unguja na Pemba kuelezea juhudi za mazungunzo
yakisiasa yanayoendelea pamoja na hatua iliyofikiwa yaliyoanza Novemba mwaka
jana mara baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, ambapo tume ya uchaguzi Zanzibar
ilimtangaza Dk. Mwinyi kuwa mshindi jambo lililopigwa na ACT kwa madai kwamba uchaguzi uligubigwa na
hila , wizi wa kura na udanganyifu.
Mwisho.
Imetolewa
na Ofisi ya Mwenyekiti wa Taifa wa ACT leo Jumapili Februari 15, 2026.


0 Comments