Na. Peter Haule, WF, Dodoma
Naibu Katibu Mkuu (Huduma za Hazina) Wizara ya Fedha, Bw. Nsubili Joshua, amewataka Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara hiyo kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa bidii, weledi na kwa kuzingatia muda, ili kuhakikisha Wizara inatoa mchango mkubwa na wenye tija katika maendeleo ya Taifa.
Bw. Joshua ametoa wito huo wakati wa kikao kazi na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara (Fungu 50) kilichofanyika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.
Amesisitiza umuhimu wa uwajibikaji, ushirikiano na ubunifu katika utekelezaji wa majukumu ya kila siku, ili kuongeza ufanisi na kufikia malengo yaliyowekwa.
Kwa upande wao, Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara ya Fedha (Fungu 50) wameahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na mshikamano, pamoja na kuahidi kumpa ushirikiano wa kutosha kiongozi huyo, ili kuhakikisha utekelezaji mzuri wa majukumu ya Wizara, ikiwemo usimamizi wa sera za uchumi na programu mbalimbali za maendeleo.
Naibu Katibu Mkuu Huduma za Hazina Wizara ya Fedha, Bw. Nsubili Joshua, akipokelewa na baadhi ya Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara hiyo Fungu 50 na watumishi kabla ya Kikao kazi na Watendaji hao katika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.
.jpg)
.jpg)

.jpg)
0 Comments