Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Rais wa
Angola ambaye pia Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) Mhe. João Lourenço, Rais
wa Jamhuri ya Ghana Mhe. John Mahama wa pili kutoka (kushoto), Waziri
Mkuu wa Msumbiji Mhe. Maria Benvinda Levy wa kwanza (kushoto), Mwanzilishi
Mwenza na Mwenyekiti Mtendaji wa GAIS na Rais Mstaafu wa Benki ya Maendeleo ya
Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina pamoja na Mwanzilishi na Mwenyekiti
Mtendaji wa APCO Worldwide, Bi. Margery Kraus wa kwanza (kulia) mara
baada ya uzinduzi rasmi wa Jukwaa la Uwekezaji barani Afrika (GAIS),
uliofanyika Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu tarehe 03 Februari, 2026
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akihutubia
katika uzinduzi wa Jukwaa la Uwekezaji barani Afrika (GAIS), Dubai, Umoja wa
Falme za Kiarabu tarehe 03 Februari, 2026.Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, jana usiku alishiriki uzinduzi wa Global Africa Investment Summit (GAIS) jijini Dubai, tukio lililoashiria hatua mpya ya Afrika katika kuvutia mitaji ya kimataifa kupitia uwekezaji uliopangiliwa na wenye uhalisia wa kifedha.
Akihutubia mkutano huo, Mhe. Rais alisisitiza kuwa wawekezaji hawatafuti fursa pekee, bali uaminifu - uthabiti wa sera, taasisi imara na serikali zinazotekeleza ahadi zake. Alieleza namna Tanzania imewekeza kimkakati katika nishati, reli, bandari na miundombinu ya uchukuzi, pamoja na Maeneo Maalum ya Uwekezaji na Dirisha Moja la Uwekezaji, ili kujenga mazingira rafiki kwa wawekezaji wa muda mrefu.
Ushiriki wa Tanzania katika GAIS unaakisi dhamira ya nchi ya kwenda kwenye ushirikiano uliopangiliwa vizuri na unaoendana na vipaumbele vya maendeleo ya taifa na matarajio ya wawekezaji wa kimataifa.
GAIS inalenga kuoanisha uongozi wa kisiasa, rasilimali za kitaifa na mitaji ya kimataifa, na kuifanya Afrika - na hususan Tanzania - kuwa kitovu cha uwekezaji unaoleta matokeo, ajira na maendeleo endelevu.
#GAIS2026
#EconomicDiplomacy
#KaziNaUtuTunasongaMbele



0 Comments