Katika kuadhimisha miaka 48 ya Mapinduzi ya Zanzibar, Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Zanzibar, inakusudia kuendesha michuano ya mpira wa miguu katika kusherehekea siku hiyo adhimu.
Hivyo katika kufanikisha azma hiyo, WHUUM imeunda Kamati maalum ya watu wanane (8) watakaokuwa na jukumu la kusimamia michuano hiyo, lengo la awali likiwa ni kutafuta fedha ya kuendesha michuano hiyo.
Wahusika katika Kamati hiyo ni pamoja;-
1.Mhe. Mohammed Hassanali Raza – M/kiti
2.Sharrifa Khamis (Makamu Mwenyekiti).
3.Nd. Amaan I. Makungu – (Mshika fedha)
4.Nd. Khamis A. Said – (Katibu).
5.Nd. Nassor A. Salim – Mjumbe
6.Nd. Tawfiq Salim Turky - Mjumbe
7.Nd. Abubakar Said Bakhresa – Mjumbe
8.Nd.Al-halil Mirza – Mjumbe
Hii ni kwa taarifa, maelezo zaidi ya maandalizi ya michuano hiyo itafuata.
………………….
Abdi Sh, Abdullah
AFISA UHUSIANO - WHUUM
No comments:
Post a Comment