Habari za Punde

Nabii Aliyepiga Teke Sadaka Aanguka Kanisani

Alikuwa akiendesha sala kuwalaani waandishi

Joseph Ngilisho, ARUSHA


NABII Benjamin Asaf ameanguka hafla kanisani wakati akioendesha sala ya kuwaombea laana waandishi wa habari na waumini wa kanisa lake.

Nabii huyo wa kanisa la huduma ya mti wa uzima madhehebu ya Ebenezer Gospel Church lilioko Mererani, alikuwaa akiendesha sala ya kuwaombe waumini wake waliotoa habari kwa waandishi juu ya kadhia ya kuwanyanyasa na kupiga teke sadaka akidai kidogo.

Aidha sala hiyo pia ililenga kuwaombea laana waandishi wa habari waliojitia kimbelembele cha kuandika habari hizo, ambapo kabla ya kumaliza sala hiyo alidondoka chini.

Wakizungumza na waandishi wa habari kwa sharti la kutotajwa majina yao, waumini hao walisema kuwa mchungaji huyo alianguka ghafla kwenye madhabahu ya kanisa hilo.

Walisema wakatia kiingia kanisani alikuwa akisema leo kazi ni moja tu ya kuendesha maombi ya kuwalaani waandishi wa habari wote walioandika habari zake.

“Wakati akiendelea kuomba huku akiwa ameshikilia bibilia ghafla alianguka chini na kupoteza fahamu kwa muda na baadae waumini hao walimpepea ambapo aliinuka ila hakuendelea tena na maombi”,alisema mmoja wa waumini aliyekuwepo kanisani hapo.

Waumini hao walisema inawezekana laana aliyokusudia iwafike waandishi wa habari na baadhi ya waumini waliovujisha siri za kanisa hilo juu ya kadhia ya kuvunja madhabahu na kupiga teke kikapu cha sadaka, imemrejea mwenyewe.

Waumini hao walisema mhubiri huyo anayejiita nabii, amewatendea kosa kubwa kupiga teke sadaka zao walizozitoa kwa ajili ya Mungu na kuvunja madhabahu yao.

Aidha walisema nabii huyo aliwatolea maneno ya ujeuri baada ya kuvunja madhabahu kwa kuwataka mabaki wakapikie makande na kueleza kuwa sakada wanazotoa kidogo ndio maana mchungaji wao Joshua Baraka hanenepi.

Wamesema katika ibada iliyofanyika wiki iliyopita kwenye dhehebu lao Nabii huyo aliwaita waumini hao wadudu, kunguni na mende  na kuwauliza kuwa kwanini walipeleka jambo hilo kwenye vyombo vya habari.

Mmoja kati ya waumini hao ambaye alikuwa na mtoto mdogo wakati tukio hilo linafanyika alisema alisikia uchungu kuona sadaka aliyoitoa kwa ajili ya Mungu kwanini ipigwa teke.

Alisema wakati Nabii huyo akipiga teke kapu la sadaka, noti ya shilingi 1000 ilimrukia mguuni mwake ndipo alipoamua kuichukua na kuiweka kwenye pochi na kuamua kuhama kanisa hilo na hadi hivi sasa amehamia kanisa la huduma ya Haradali.

Hata hivyo, waumini hao wameshangazwa na kitendo cha wao kusimangwa na na mtu huyo anayejiita nabii na kudai kuwa wao wamenenepeana huku mchungaji wao Baraka Joshua akiwa amekonda.

Walisema uongozi wao unatakiwa kugeuka kwani kitendo hicho cha kupiga teke sadaka na kuvunja madhabahu kinafanana na waamini wa kule Mbeya ambao hivi karibuni nao walivunja madhabau yao wakitafuta madini yaliyohifadhiwa na wamisionari.




No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.