Na
Mwandishi wetu
IMETHIBITIKA
kuwa watu 9 wamefariki dunia na wengine 12 hawajulikani waliko baada ya boti ya
abiria kuzama katika Ziwa Tanganyika
nchini Tanzania.
Taarifa
zinasema kuwa, boti hiyo ilizama baada ya kukumbwa na dhuruba ambapo watu
wengine 64 wameokolewa.
Kamanda
wa Polisi wa mkoa wa Kigoma, Fraiser Kashai amethibitisha hayo na kusema kuwa
boti hiyo inayoitwa 'Tunusuru Yarabi' ilikuwa ikitokea Kirando mkoani Rukwa
ikielekea katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo
kupitia Rumonge Burundi
na ilikuwa imebeba abiria, shehena ya dagaa, vyakula na bidhaa za viwandani.
Baadhi
ya abiria walionusurika waliokuwa wakisafiri na boti hiyo wamesema, pamoja na
kuwa dhuruba ndiyo iliyosababisha ajali hiyo lakini shehena kubwa ya vitu
mbalimbali vilivyokuwa vimebebebwa vilichangia kuzama boti hiyo.
No comments:
Post a Comment