Na Fatuma Kitima,Dar es Salaam
TUME ya Mabadiliko ya Katiba imewakubalia watu
wenye ulemavu kuunda baraza lao la katiba ambalo litakuwa likipitia rasimu ya
katiba ambayo itatolewa na tume hiyo.
Akizungumza Dar es
Salaam jana, Mwenyekiti wa maandalizi wa
kamati ya Umoja wa Wajasiriamali walemavu Mkoa wa Dar es Salaam (UWAWADA),
David Nyendo alisema kukubali kwa tume hiyo ni neema kwa wenye ulemavu kusimamia haki zao katika katiba
mpya.
Alisema Mwenyekiti
wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji mstaafu,
Joseph Warioba amekiri kuwa suala la watu wenye
ulemavu kuwa na baraza la katiba lilikuwa halipo katika mlolongo wa
mabaraza yatakayoundwa.
Alisema kuanzia
sasa wanajipanga na kuhamasisha mabaraza
ya watu wenye ulemavu kila wilaya ambao ndio muungozo wa kusimamia haki za watu
wenye ulemavu katika katiba mpya.
Aidha alisema walemavu
wamefarijika kuwepo kwa baraza la watu
wenye ulemavu katika kila wilaya kutokana
na tume kujua umuhimu wao kushiriki katika mchakato huo.
Hata hivyo,
alisema ushiriki wao katika mabaraza hayo utasaidia kupata katiba ambayo
itakayokuwa inatambua haki zao.
Naye Mwenyekiti wa Umoja wa wajasiriamali Wenye
Ulemavu Mkoa wa Dar es Salaam, Kidumke Mohamed alisema watu ambao watachaguliwa
katika mabaraza hayo wawe makini kuangalia vitu ambavyo vinawahusu watu wenye
ulemavu na kuvisimamia kuingizwa katika katiba mpya.
No comments:
Post a Comment