Na: Abdi Suleiman, PEMBA.
Katika hali isiyo ya kawaida wachezaji wanne wa 
timu ya Yanga, wameshindwa kufanya mazoezi na 
wenzao kwa sababu mbali mbali.
Yanga ambayo ipo Pemba kwa ajili ya maandalizi ya 
mchezo wao na Azam FC wa ligi kuu ya 
sokaTanzania bara, utapigwa katika uwanja wa taifa 
wikiendi hii.
Wachezaji hao ambao wameshindwa kuungana na 
wenzao ni Saimon Msuva, Salum Telela, Nadir 
Haroub Kanavaro na Amis Tambwe ambaye 
hakuonekana kabisa kiwanjani hapo.
Saimon Msuva na Salum Telela waliweza kuungana 
na wenzao katika kuomba dua, badala yake wakakaa 
pembeni na kuwaachia wenzao kuendelea na 
program zao, huku kocha mkuu Hans Van Plujin 
akiwataka kukimbia uwanjani humo.
Saimon Msuva alilazimika kukaa chini baada ya 
kushindwa kuendelea na mazoezi mepesi ya 
kukimbia na kumwacha Telela akimaliza raundi 
zisizopungua 15.
Kufuatia hali ya majeruhi kuanza kuindama Yanga, 
imemfanya kocha wa timu hiyo kuwa makini katika 
mazoezi yanayoendelea katika uwanja wa Gombani.
Wakati huo huo timu hiyo imelazimika kubadilisha 
ratiba ya mazoezi iliyokuwa ikiifuata kila siku tokea 
kuwasili kisiwani Pemba, ambapo leo timu hiyo 
imefanya mazoezi yake asubuhi majira ya saa nne 
kamili kijuwa kikali kikiwaka.
Yanga imeonekana kuukamia vikali sana mchezo huo 
dhidi ya Azam, kwani inataka kujihakikishia 
inawakimbia kwa masafa marefu wapinzani wao, 
huku kesho baada ya mazoezi inatarajiwa kuondoka 
kisiwani Pemba kurejea Tanzania bara.
 

 
.jpeg) 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment