Habari za Punde

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Afanyac Ziara Kisiwani Pemba.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe Charles akiwa katika ziara yake Kisiwani Pemba akitembelea maeneo ya Mji wa Chakechake akiwa Wakuu wa Mikoa wa Pemba Mhe Mwanajuma Majid na Omar Khamis Othman wakiwa katika ziara ya Mhe Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi wakati wa ziara yake kisiwani humo.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe:Charles Kitwanga, akizungumza na wananchi waliofika katika Hospitali ya Chake Chake kuwajulia hali jamaa zao, wakati wa ziara yake kisiwani Pemba kuangalia hali ya amani na Utulivu Ilivyo
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe:Charles Kitwanga, akizungumza na wafanya biashara wadogo wadogo wa nguo waliopo katika soka la matunda Chake Chake, wakati wa ziara yake kisiwani Pemba kuangalia hali ya amani na utulivu ilivyo 
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe:Charles Kitwanga, akizungumza na askari Polisi katika kituo FFU Finya, wakati wa ziara yake kisiwani Pemba kuangalia hali ya amani na Utulivu Kisiwani Pemba.
MKUU wa Mkoa wa kusini Pemba Mhe:Mwanajuma Majid Abdalla, akizungumza na askari polisi katika kituo chao cha FFU Finya, wakati wa ziara ya Waziri Charles Kitwanga wakati wa ziara yake kisiwani Pemba
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe:Charles Kitwanga, akizungumza na maafisa wa Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba katikati ni kamanda wa Polisi Mkoa huo Hassan Nassir Ali, wakati alipofika katika msitu wa ngezi Wilaya ya Micheweni.
MKUU wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Mhe:Omar Khamis Othaman, akitoa maelezo kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Charles Kitwanga, juu ya kuwepo madai wananchi wamekimbilia katika msitu wa ngezi Wilaya ya Micheweni
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe:Charles Kitwanga, akizungumza na waandishi wa habari kisiwani Pemba, mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku moja kisiwani hapa, kuangalia hali ya Ulinzi na Usalama kisiwani humo
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe:Charles Kitwanga, akiwa na Mkuu wa Mkoa wa kusini Pemba Mhe:Mwanajuma Majid Abdall, Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Mhe;Hemed Suleiman Abdalla, wakiangalia meli ya Mv Serengeti wakati ikiwasili kisiwani Pemba katika bandari ya Mkoani ikitokea Unguja.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe:Charles Kitwanga, akizungumza na vijana wanaobeba mizigo katika bandari ya Mkoani, wakati alipofanya ziara katika bandari hiyo huku meli ya mv Serengeti ikiwa inawasili ikitokea kisiwani Unguja.
(Picha na Abdi Suleiman, Pemba)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.