Na
Abdi Shamnah
WASHIRIKI
wa mkutano unaojadili rasimu ya Sera ya Taifa ya usimamizi wa uvuvi wa bahari
kuu Tanzania, wametakiwa kujadili rasimu hiyo kwa kina, ili kufanikisha dhamira
za serikali, za kuwa na sera madhubuti itakayoweza kusimamia vyema uvuvi wa
bahari kuu.
Changamoto
hiyo imetolewa leo na Naibu Katibu Mkuu (anaeshugulikia mifugo na uvuvi), Dk.
Islam Seif, katika ufunguzi wa mkutano wa wadau wa uvuvi, unaojadili rasimu ya
sera ya Taifa ya usimamiziwa uvuvi wa
bahari kuu, uliofanyika katika ukumbi wa Mamlaka ulioko Fumba.
Mkutano
huo umewahusisha wadau na wataalamu wa
sera na watafiti kutoka taasisi za serikali na asasi za kiraia, ikiwemo idara
ya Uvuvi, Mazingira,vyama vya mabaharia, ZMA, SUMATRA, TPA, ZPC, wamiliki wa viwanda vya kusindika samaki, vyuo
vya uvuvi na NGO mbali mbali.
Alisema
Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya Zanzibar, zina matarajio
makubwa kuwa mkutano huo utatoka na sera madhubuti itakayoweza kusimamia vyema
uvuvi wa bahari kuu, ili kuleta tija ya kijamii na kiuchumi kwa taifa na
wananchi wake.
Alisema
ni jukumu la wadau hao kujadili kwa kina rasimu hiyo ili kufikia malengo ya
kuanzishwa Mamlaka hiyo yenye azma ya
kukuza, kusimamia na udhibiti uvuvi wa
bahari kuu.
Aidha
aliwataka wadau hao kuzingatia mambo ya
msingi yatakayoipa sifa sera hiyo, ikiwemo uimarishaji uwezo wa kifedha, miundombinu
na uhifadhi wa mazingira ya ukanda wa kiuchumi.
‘‘Sera
inapaswa kuzingatia utekelezaji wa mipango ya usimamizi wa uvuvi, leseni
ziendane na rasilimali zinazovunwa pamoja na kuhakikisha kunakuwepo
ushirikishwaji wa wazawa katika uvuvi wa bahari kuu’’, alisema.
Dk.
Islam alibainisha kuwa katka kufanikisha azma ya Serikali ya kuwa na uchumi wa
viwanda, kuna haja ya kuzingatia upatikanaji wa ajira kupitia viwanda na
masoko.
‘’
Lakini pia sera iainishe fursa zilizopo katika uanzishaji wa aina nyengine za
uvuvi, sambamba na namna ya kujenga mawasiliano na kumarisha mashirikiano na sekta nyengine za kiuchumi’’,
alisema.
Nae,
Mshauri mwelekezi Dk. Indu, ambae anashirkiana na serikali kuandaa sera hiyo, aliishukuru Serikali kwa
mashirikiano yake yenye lengo la kukamilisha sera hiyo.
Alisema
kukamilika kwa sera hiyo, kutaiwezesha mamlaka kusimamia na kudhibiti vyema uvuvi katika
ukanda huo wa kiuchumi, hivyo kukidhi mahitaji ya wananchi kijamii na kiuchumi.
Aidha
alisema itafanikisha malengo ya serikali ya kufikia uchumi wa viwanda ifikapo
2025, sambamba na dira ya kupambana na umasikini.
Mamlaka
ya Usimamizi wa uvuvi wa bahari kuu, ilianzishwa mnamo 2010 na tangu hapo bado
haijawa na sera yake.
No comments:
Post a Comment