Habari za Punde

Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania TIRA, wafanya uhakiki wa Bima za vyombo vya moto kisiwani Pemba

 POLISI wa usalama barabarani wakiwa kwenye zoezi maalum la kufanya uhakiki wa bima halali kwa njia ya mtandao, mara baada ya Polisi hao kupata mafunzo ya jinsi ya utambuzi wa bima zia kughushi, hivi karibuni kisiwani Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba). 
 MTOTO Fauzi  Mohamed Subeit (16) mkaazi wa Mkoroshoni wilaya ya Chakechake, akizungumza na waandishi pamoja na Polisi wa usalama barabarani, baada ya kukamatwa akiendesha gari kinyume na sheria, wakati Polisi hao wakifanya uhakiki wa bima halali kw anjia ya mtandao, mara baada ya Polisi hao kupewa mafunzo na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania TIRA, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 GARI kadhaa zikiwemo za kutembelea, za abiria, mzigo na vyombo vya magurudumu mawili zikiwa uwanja wa Gombani Chakechake, ili kufanyiwa uhakiki wa namba za bima zao, na watendaji wa Polisi na wale kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania TIRA, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 GARI kadhaa zikiwemo za kutembelea, za abiria, mzigo na vyombo vya magurudumu mawili zikiwa uwanja wa Gombani Chakechake, ili kufanyiwa uhakiki wa namba za bima zao, na watendaji wa Polisi na wale kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania TIRA, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 MKUU wa kikosi cha uslama barabarani mkoa wa kusini Pemba Shawali Abdalla Ali, akishiriki katika zoezi la utambuzi wa bima halali, akiwa na watendaji wengine kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania ‘TIRA’ ambapo vyombo vya usafiri 71 walivigundua havina bima halali katika 168 walivyovihakiki, (Picha na Haji Nassor, Pemba)
BAADHI ya abiria walikuwa wakisafiri na gari mbali mbali za abiria, wakilazimika kutembea kwa miguu wakiwa na mizigo yao, baada ya gari walizokuwa wamepanda kufanyiwa uhakiki wa bima zao na kugundulika kuwa ni za kughushi, kwenye zoezi maalumu lililofanywa na Jeshi la Polisi na Mamlaka ya usimamizi wa bima Tanzania TIRA, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

 BAADHI ya abiria walikuwa wakisafiri na gari mbali mbali za abiria, wakilazimika kutembea kwa miguu wakiwa na mizigo yao, baada ya gari walizokuwa wamepanda kufanyiwa uhakiki wa bima zao na kugundulika kuwa ni za kughushi, kwenye zoezi maalumu lililofanywa na Jeshi la Polisi na Mamlaka ya usimamizi wa bima Tanzania TIRA, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 WATENDAJI wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania TIRA, wakilifanyia uhakiki gari linalomilikiwa na Kampuni na Bakhersa Food Products, iwapo bima yake inatambulika, wakati wa zoezi hilo maalum lililofanyika hivi karibuni kisiwani Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba) 
 DEREVA wa gari ya abiria ambae hakupatikana jina lake, akielezea mtazamo wake juu ya zoezi la uhakiki wa bima halali, lililofanywa na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na watendaji wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania TIRA, hivi karibuni kisiwani Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).  

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.