HABIBA ZARALI, PEMBA
Umoja wa Jumuiya zisizo za kiserikali Pemba (PACSO), umepata
viongozi wapya, kufuatia Mkutano mkuu wa Jumuiya hiyo, uliofanyika katika skuli
ya Maandalizi Madungu mjini Chakechake kwa kuwachagua viongozi wapata watakaoiongoza
Jumuia hiyo kwa miaka mitano.
Waliochaguliwa ni pamoja na Omar Ali
Omar kuwa Mwenyekiti, Mohamed Ali Khamis kuwa Makamo Mwenyekiti, Sifuni Ali
Haji amechaguliwa kuwa Katibu Mkuu huku Mshika Fedha akichaguliwa Is-haka Asaa
Hamad.
Kwa upande wa wajumbe wa kamati
tendaji, waliochaguliwa ni Juma Ali Mati Mkoani, Ali Shomari Chake Chake, Ali
Kombo Mali, Asha Pandu, Othman Hamad na Fadhila Khamis wa Micheweni.
Akizungumza na gazeti hili mara baada
ya kuchaguliwa Katibu mkuu mpya Sifuni Ali Haji, alisema ushirikiano mazuri
kati ya taasisi nyengine na PACSO, ndio njia ya msingi ya kiziwezesha asasi za
kiraia, kuwapeleka mbele na kuwaletea maendeleo.
Alisema wakati umefika kwa asasi za
kiraia kuwa bega kwa bega na jumuiya ya ‘PACSO’ ili kuweza kufanya mambo
yanayoweza kuwasogeza mbele katika harakati za kazi zao.
Aliitaja mikakati aliyonayo wakati wa
uongozi wake, alisema ni kuzishirikisha asasi za kiraia kwa kudumisha umoja na
kuleta maslahi katika asasi hizo na kuandaa kamati za taaluma na ufuatiliaji kama ulivyopangwa.
“Ntahakikisha natatekeleza mazuri na
kudumisha umoja na mshikamano katika taasisi zote, ili umoja huu uzidi kusonga
mbele na kuweza kuleta faida kwa yale yaliokusudiwa”,alisema.
Katibu Mkuu huyo aliziomba taasisi
mbalimbali kuachana na dhana potofu ya kuwa ‘PACSO’ haina faida na kuwataka kujiunga
na uwanachama, ili kuweza kuzidisha nguvu na kujiletea maendeleo katika taasisi
zao.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya
hiyo Omar Ali Omar, alisema ni vyema kwa
asasi hizo zikawa na upendo utakaowaonesha njia sahihi katika kujitafutia fursa
mbalimbali za kimaendeleo.
Alisema wakati umefika wa kuondowa
tabia ya kulaumiana na kulalamikia jambo lisilo na msingi ndani ya asassi zao badala
yake wachukuwe juhudi binafsi za kurekebisha
panapohitajika.
“Pale ambapo asasi moja itaona kwamba
kuna fursa mahali fulani basi iweze
kuitaarifu na asasi nyengine ili kwa
umoja huu uweze kutekeleza majukumu na malengo yaliowekwa”,alisema.
Mapema akielezea miongoni mwa
mafanikio yaliyopatikana katika jumuiya hiyo, Katibu Mkuu aliyemaliza muda wake
Mohamed Najim Omar, alisema ni pamoja na jumuiya kuongeza idadi ya wanachama
kutoka 77 hadi kufikia 84, kupata bodi ya wadhamini.
Alisema miongoni mwa changamoto
zinazoikabili jumuiya hiyo ni pamoja na ulipaji mdogo wa ada kwa wanachama
kwenye mtandao, ukosefu wa mfanyakazi wa kudumu
anaeweza kushughulikia harakati za kila siku za ofisi, ili aweze kuwapatia taarifa
wanaohusika na kutokuwa na ofisi ya kudumu.
Mtandao wa asasi za kiraia kisiwani
Pemba una mashirikiano na wadau mbalimbali, ikiwemo watu binafsi ,sekta za umma
na asasi mbalimbali katika wilaya zote za Pemba, kwa lengo la kuleta umoja na
maendeleo ya wananchi kwa kuzididisha nguvu za pamoja.
No comments:
Post a Comment