Makamo wa pili wa Rais wa Zanzibar balozi Seif Ali Iddi akipokea msaada wa fedha taslim shillingi milioni 10 kutoka kwa mchungaji Bariki Urassa wa madhehebu ya Efatha kwa ajili ya hospitali ya rufaa ya Mnazi Mmoja
Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar balozi Seif Ali Iddi akionyesha msaada huo wa fedha taslimu kwa waandishi wa habari waliohudhuria hafla hiyo ambayo pia ilihudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya ndugu Asha Ali Abdallah(Picha na OMPR)
Na. Mwandishi OMPR.
Makamo wa pili wa Rais wa
Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amesema utamaduni wa watu wa Zanzibar wa
kuheshimu dini zote ni nguzo imara iliyosimamisha amani na utulivu nchini.
Balozi Seif ameyasema hayo
afisini kwake Vuga wakati akipokea msaada wa fedha taslim shilingi milioni 10
kwa ajili ya sekta ya afya kutoka kwa mchungaji Bariki Urassa wa madhehebu ya
Efatha nchini.
Amesema tangu zamani
waumini wa dini ya Kikristo na Kiislamu wamekuwa wakiishi pamoja na kushirikiana
katika mambo mbali mbali ya kijamii bila ya mikwaruzano.
Amesema msaada huo wa fedha
ambao umekusudiwa kwa hospitali ya Rufaa ya Mnazi Mmoja umekuja wakati muwafaka
ambapo Serikali imo katika mipango ya kuimarisha huduma zote zitolewazo
hospitalini hapo.
Akikabidhi msaada huo wa
shilingi milioni 10 kwa Makamo wa Pili wa Rais, mchungaji Bariki Urassa amesema
madhehebu yao ya Efatha hupeleka misaada yake pale inapohitajika.
Amesema wakati wa ziara ya
kiongozi wao Mkuu wa Efatha Duniani mchungaji Josephate Elias Mwingira
alipoonana na makamo wa Pili wa Rais aliahidi kuisaidia Hospitali ya Mnazi
Mmoja, ahadi ambayo amekuja kuitekeleza kwa niaba yake.
Sherehe fupi ya
makabidhiano ya msaada huo ilihudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya ndugu
Asha Ali Abdallah ambaye kwa niaba ya Wizara yake ameahidi kuutumia msaada huo
kama ulivyokusudiwa.
Katibu Mkuu huyo amesema
Wizara yake itatoa mashirikiano ya karibu kwa wale wote wanaotaka kuchangia na
kutoa wito kwa taasisi nyengine za ndani na nje kujitokeza kutoa misaada yao kwa
Wizara yake ambayo imepewa majukumu makubwa ya kuwahudumia kifya wananchi wote
wa Zanzibar.
No comments:
Post a Comment