Habari za Punde

NJIA TANO ZA KUILINDA SIMU YAKO YA ANDROID

Na Jumia Tanzania.
Kama unamiliki simu inayotumia mfumo wa Android, basi hautakiwi kijisahau hususani juu ya masuala ya usiri wa matumizi yako na usalama. Hususani kama simu yako ya Android haipati maelekezo ya kusasisha mifumo ya kiusalama mara kwa mara kama watumiaji wa iPhone. Kumiliki simu ya Android inamaanisha kwamba unatakiwa kuwa na umakini wa ziada hususani kwenye progaramu unazozipakua mtandaoni, aina ya mafaili ya APK unayoyaweka kwenye simu yako, kuwa mwangalifu na watengeneza programu wanaozitoa bure. 
Kwa kuwa watumiaji wa Android hawapati fursa ya kujulishwa kuhusu kusasisha usalama wa simu zao kwa mwezi au wiki, kuna hatua muhimu za kufuata ili kuifanya simu yako ya Android kuwa imara dhidi ya mashambulizi kutoka nje - programu zinazolenga kudhuru au kuharibu na kudukua mifumo ya simu. Kuna njia kadhaa za kuilinda simu yako ya Android dhidi ya mashambulio hayo ambayo Jumia ikiwa inajiandaa kuwalete ‘Wiki ya Simu’ wateja wake ingependa kukujulisha kama ifuatavyo:

Funga Skrini Yako. Hili linaweza kuonekana ni jambo la kawaida lakini linaweza kuisaidia simu yako dhidi ya kutumiwa bila ya ruhusa yako au kuwa salama wakati haupo karibu nayo. Iwe umetoka mara moja au umeiacha simu yako mezani unapofanyia kazi, kuiwezesha simu yako kujifunga pindi hauna matumizi nayo kama vile kuweka nenosiri, kufunga kwa kutumia mchoro, uso au namba za siri kunakupatia usalama wa taarifa na kumbukumbu zako kwa hali ya juu.         
Funga Programu na Mafaili Unayoyatumia. Utaratibu unaweza kuuona kama unachosha lakini ipo siku utakuja kuutambua umuhimu wake pindi programu zako zitakopodhuriwa au kuharibiwa na virusi kwenye kompyuta. Kuna programu kadha wa kadha kwenye ‘Play Store’ ambazo zinaweza kukusaidia kufunga programu na mafaili yako moja baada ya nyingine na kuzilinda dhidi ya kuharibiwa, kudukuliwa, kuharibiwa na virusi pamoja na madhara mengine.

Pakua Programu Kutoka ‘Google Play Store’ Pekee. Unapoweka programu kwenye simu yako, kuna mahala oanakuonyesha kuweka chaguo la kuruhusu kuweka programu kutoka kwa wanaprogramu wasioruhusiwa, hakikisha kwamba sehemu hiyo inaonyesha ‘No’ au ‘Off’ inategemea na mfumo wa android yako. Sehemu hii inatakiwa kuonyesha kutoruhusu, hali hiyo itaifanya simu yako kutoweka programu ambazo hazijaidhinishwa kwenye ‘Google Play Store’. Kupakua na kuweka programu ambazo hazijulikani zimetengenezwa nani, kunaweza kuiweka simu yako kwenye hatari kubwa. Ni muhimu sana kupakua programu kupitia ‘Play Store’ pekee!

Sasisha (Update) Programu zako. Kusasisha au kuzifanyia maboresho programu kwenye simu yako kila mapendekezo kutoka kwa wanaprogramu walioziunda ni muhimu sana. Kila maboresho huja kurekebisha kasoro fulani au kukifanya kifaa chako kuwa imara zaidi. Wanaprogramu hugundua kasoro ndogondogo zinazofanya programu zilizopo sasa kutanya kazi kwa ufanisi, baadhi huwa ni za kiusalama, wanazifanyia kazi, wanazirekebisha na kisha kuziruhusu kupatikana kwa watumiaji kupitia kwenye matoleo yenye maboresho mapya. Hivyo, kama una toleo la programu lililopitwa na wakati kwenye simu yako, ni vema ukazifanyia marekebisho ili kupunguza hatari ya simu yako kuwa hatarini kushambuliwa.

Sasisha Android OS. Toleo la hivi karibuni la android ni Android 8 Oreo. Hakuna shaka kwamba kila toleo jipya la mfumo wa ufanyaji kazi wa simu ya Android huja na maboresho zaidi ya usalama. Iwapo bado unatumia mfumo uliopitwa muda wa android os, upo hatarini kushambuliwa, kuharibiwa, kudukuliwa na hatari zingine tofauti kwenye simu yako. Endapo simu yako haikubali toleo jipya la maboresho ya android os, ni wakati wako kuhifadhi taarifa zako kwenye mfumo wa ‘google drive’ na kuanza kupanga namna ya kupata kifaa kipya chenye toleo la hivi karibuni la OS au angalau kinachotumia Android 7 Nougat.     



No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.