RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amempongeza Makamo wa Pili
wa Rais Balozi Seif Ali Idd kwa kumsaidia kazi na kuendelea kuisimamia vyema
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais.
Dk. Shein aliyasema
hayo, Ikulu mjini Zanzibar alipokutana na uongozi wa Ofisi ya Makamu wa Pili wa
Rais wakati ilipowasilisha utekelezaji wa Mpango Kazi wa Mwaka 2017/2018, na Mpango
Kazi wa Utekelezaji kwa mwaka 2018/2019.
Dk. Shein alitumia fursa hiyo kumpongezi kwa
Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali
Idd kwa kumsaidia kazi pamoja na
kuupongeza uongozi wa Ofisi hiyo na watendaji wake kwa kufanya kazi
zinazoonekana na zisizoonekana zikiwemo Mazingira na UKIMWI.
Pia, alimpongeza Waziri, Naibu Waziri na watendaji
wengine wote wa Ofisi hiyo kwa kazi nzuri wanazoendelea kuzifanya ndani ya
Ofisi hiyo pamoja na nje ya Ofisi hiyo ikiwemo katika Baraza la Wawakilishi la
Zanzibar.
Pamoja na
hayo, Rais Dk. Shein alisisitiza haja ya usimamizi katika utekelezaji wa
majukumu ya kazi hatua ambayo huleta
ufanisi mkubwa pamoja na uwajibikaji kazini.
Alieleza kuwa kuanzishwa kwa taasisi za utafiti ambazo
zimeundwa kwa mujibu wa Sheria kuna umuhimu mkubwa katika kufikia malengo
yaliokwekwa juu ya suala zima la tafiti hapa Zanzibar.
Rais Dk. Shein alisisitiza kuwa upimaji wa UKIMWI ni
jambo la hiyari hivyo alitoa wito kwa uongozi
huo kuendelea kutumia utamaduni wa kuwashajiisha wananchi kwenda kupima badala
ya kuwalazimisha.
Hivyo, Dk. Shein alisisitiza haja ya kutoa elimu kwa
jamii juu ya suala zima la kupima UKIMWI hatua ambayo itasaidia kwa kiasi
kikubwa kufikia malengo yaliokusudiwa.
Pamoja na hayo, Rais Dk. Shein aliendelea
kusisitiza haja na wajibu kwa kiongozi katika kusimamia na kuwajibika katika
utendaji wa kazi.
Nae Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi
Dk. Abdulhamid Yahya Mzee aliupongeza uwasilishaji Mpango Kazi na utekelezaji
wake uliofanywa na Wizara hiyo na kusisitiza haja ya kwa uongozi wa Ofisi hiyo
kuendelea kujenga taswira nzuri na kuwa mfano kwa wengine.
Mshauri wa Rais Ushirikiano wa Kimataifa na Uchumi
Balozi Mohamed Ramia Abdiwawa alieleza
kuwepo kwa Kitengo cha kufuatilia maagizo na maelekezo ya Serikali ambacho
tayari kimeshaanza kazi hivyo
mashirikiano yanahitajika kwa uongozi wa Wizara zote za Serikali na taasisi
zake ili kufanikisha majukumu hayo.
Mapema Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa
Pili wa Rais Zanzibar, Mohamed Aboud
Mohamed alitoa pongezi na kumshukuru
Rais Dk. Shein kwa kuendelea kuiongoza vyema Zanzibar na kusimamia ipasavyo
utendaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kutoa huduma bora kwa
wananchi na kuwaletea maendeleo.
Uongozi huo ulitoa shukurani kwa Rais Dk. Shein
kwa maelekezo na miongozo anayowapa ambayo imesaidia sana katika kutekeleza
majukumu yao kwa wananchi.
“Tunamuomba Mola akuzidishie hekima, busara na
afya njema ili uzidi kutuongoza”, alisema
Waziri Aboud.
Aidha, uongozi wa Ofisi hiyo juhudi zake katika kupambana na dawa za
kulevya ambapo Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya
Zanzibar imeendesha mafunzo kwa Wahusika wa Madiko katika Shehia zenye bandari
zisizo rasmi, kuteketeza dawa kutoka katika sehemu zilizo hifadhiwa pamoja na kufanya
shughuli nyenginezo.
Pia, Uongozi huo ulieleza mikakati iliyoiwekwa katika kupiga
vita dawa za kulevya hapa Zanzibar pamoja na mashirikiano yaliopo kati yake na
taasisi ziliopo nje ya Zanzibar katika kupambana na kadhia hiyo.
Katika maelezo pia, Waziri Aboud alimuhakikishia
Rais Dk. Shein kuwa juhudi za makusudi zitaendea kuchukuliwa katika kuhakikisha
elimu inatolewa juu ya suala zima la UKIMWI na maambukizi yake.
Pia, uongozi huo hatua zinazoendelewa kuchukuliwa
katika kuhakikisha Miongozo ya miundombinu rafiki ambayo iko katika hatua ya
mwisho kutekelezwa na huku ikiwekwa mikakati katika kuhakikisha jamiii
inahamasika juu ya suala hilo kwa lamkuhakikisha mioundombinu ina kuwa rafiki
kwa watu wenye ulemavu.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail:
rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment