Habari za Punde

Waziri wa Mambo ya Nje wa Falme za Kiarabu Azungumza na Waandishi wa Habari Zanzibar Wakati wa Ziara Yake.

Waziri wa Nchi na Ushirikiano wa Kimataifa wa Muungano wa Falme za Kiarabu (UAE)Reem Ibrahim Alhashimy  akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya kumaliza Mkutano   uliowakutanisha Viongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wakiongozwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe,Issa Haji Ussi na  Ujumbe wa Wataalamu kutoka Nchi za Falme za Kiarabu kuhusiana na mambo mabalimbali  na sekta mbalimbali ambazo wanaweza kusaidia mkutano uliofanyika Hoteli ya Park Hyyat Shangani mjini Zanzibar.

Na Faki Mjaka-Maelezo Zanzibar
Serikali ya Falme za kiarabu (UAE) inatarajia kufungua 
Ubalozi wake mdogo Zanzibar kabla ya kumalizika Mwaka 
2018 ikiwa ni mwendelezo wa kuimarisha mahusiano ya 
kidugu katika nchi hizo.
Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi na Ushirikiano wa 
Kiamataifa wa UAE, Reem Ibrahim Alhashimy 
alipozungumza na Wanahabari mara baada ya kumalizika 
kwa mkutano wa majadiliano kati ya Viongozi wa Serikali ya 
Zanzibar na UAE ukumbi wa Hotel ya Park Hyyat Mjini 
Zanzibar.  
Amesema kufunguliwa kwa Ubalozi huo kutazidisha 
mashirikiano yaliyopo na kuongeza kasi ya utekelezaji wa 
yale yaliyokubaliwa baina ya nchi hizo mbili.
Waziri Reem amesema madhumuni ya kuja Zanzibar ni 
kuihakikishia Serikali na Wananchi wa Zanzibar kwamba 
UAE ipo tayari kutekeleza yale yaliyoahidiwa katika Ziara ya 
Dkt Shein iliyofanyika nchini humo mwanzoni mwa mwaka 
huu.
Amesema kwa muda mrefu Wananchi wa UEA wamekuwa 
wakitembelea Zanzibar na kuwekeza katika maeneo mbali 
mbali kutokana na mahusiano mema yaliyojengeka miaka 
mingi.
“Binafsi sio mara ya kwanza kuja Zanzibar nimekuwa 
nikitembelea kutokana na uzuri wa Zanzibar  na watu wake 
na hivyo kuna kila sababu ya kuendelea kushirikiana katika 
mambo yetu” alisema Reem
Sekta muhimu ambazo Serikali ya ya UAE imeonesha nia ya 
kuisaidia Zanzibar ni pamoja na Sekta ya Afya, Kilimo na 
Miundombinu.
Hata hivyo hakuainisha zaidi ni eneo gani kati ya Bandari na 
Uwanja wa ndege ambalo UAE wataweza kuisaidia Zanzibar.
Kwa upande wake Wanziri wa Nchi Ofisi ya Rais na 
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Issa Haji Ussi Gavu 
amesema ziara hiyo imefungua matumaini makubwa kwa 
Zanzibar na kwamba itasaidia Zanzibar kujikwamua 
kiuchumi.
Amesema mbali na miradi iliyoombwa na Serikali ya 
Mapinduzi kwa UAE nchi hiyo pia ipo tayari kuisaidia 
Zanzibar katika miradi mingine ya ziada, ikiwemo uwezeshaji 
wa Vijana ili kukabiliana na tatizo la ajira.
Timu hiyo ya Wataalam iliwasili jana na kufanya Mikutano 
mbalimbali ya majadiliano na Viongozi wa Serikali ya 
Mapinduzi Zanzibar ikiwa ni utekelezaji wa ahadi 
mbalimbali zilizotolewa katika ziara ya Dkt. Shein 
aliyoifanya January mwaka huu katika Falme za Kiarabu.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.