Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto Jaji,Dkt.Paul
Kihwelo ambaye pia ni mratibu wa mafunzo maalumu ya kuwajengea uwezo
wa kanuni na mbinu za usuluhishi wajumbe wa Mamlaka ya Udhibiti wa
huduma za maji na Nishati Zanzibar (ZURA) akizungumza wakati wa
ufunguzi wa mafunzo hayo yanayofanyika kwenye Chuo cha Uongozi wa
Mahakama wilayani Lushoto yenye lengo la kuwajengea uwezo waweze
kufanya kazi za mamlaka hiyo kwa waledi ambapo yaliyofanyika chuoni
hapo
Mwezeshaji Jaji Mkuu Mstaafu Chande Othmani akisisitiza jambo
wakati wa mafunzo hayo
Mwezeshaji Jaji Mkuu Mstaafu Chande Othmani wa mafunzo maalumu
ya kuwajengea uwezo wa kanuni na mbinu za usuluhishi
wajumbe wa mamlaka ya udhibiti wa huduma za maji na nishati Zanzibar
(ZURA) katikati akiwa na Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufaa Jaji John
Mroso kulia na Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu Rose Temba ambaye pia ndie
mwanzilishi wa kituo cha Usuluhushi akihudumu kama Jaji Mfawidhi wa
kituo hicho wakiwa kwenye mafunzo hayo
Sehemu ya washiriki wa semina hiyo wakifuatilia kwa umakini
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wakijitambulisha
Mwezeshaji wa mafunzo maalumu ya
kuwajengea uwezo wa kanuni na mbinu za usuluhishi
wajumbe wa mamlaka ya udhibiti wa huduma za maji na nishati Zanzibar
(ZURA)Jaji Mkuu Mstaafu Chande Othmani katikati akiwa na Jaji Mstaafu
wa Mahakama ya Rufaa Jaji John
Mroso kulia na Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu Rose Temba ambaye pia ndie
mwanzilishi wa kituo cha Usuluhushi akihudumu kama Jaji Mfawidhi wa
kituo hicho wakiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki kulia wa kwanza
waliosimama ni Jaji Dkt Paul Kihwelo ambaye pia ni Mkuu wa chuo cha
Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA)
CHUO cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) leo wamefungua
mafunzo maalumu ya kuwajengea uwezo wa kanuni na mbinu za usuluhishi
wajumbe wa mamlaka ya udhibiti wa huduma za maji na nishati Zanzibar
(ZURA).
Mafunzo hayo ya siku tano yaliyoanza leo
yanafanyika kwenye Chuo cha Uongozi wa Mahakama wilayani Lushoto
mkoani Tanga yakiratibiwa na Jaji Dkt Paul Kihwelo ambaye pia ni Mkuu
wa chuo hicho.
Akizungumza wakati wa mafunzo hayo Jaji Dkt Kihwelo alisema
lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wajumbe wa bodi na viongozi
wa ZURA ili waweze kufanya kazi za mamlaka yao kwa waledi mkubwa
kuliko ilivyokuwa awali.
“Ni matumaini yetu kwamba baada
ya mafunzo watakuwa wanafahamu zaidi kanuni na mbinu mbalimbali za
usuluhishi katika maeneo yao ya kazi ikiwemo kuzifanya kwa
waledi”Alisema Jaji Kihwelo.
Aidha alisema pia pamoja naye
chuo hicho kimeandaa wakufunzi waliobobea katika eneo la usuluhishi
ili kuipa ZURA kile wanachostahili ili waweze kufahamu mbinu
mbalimbali za usuluhishi kwenye maeneo yao.
Awali
akizungumza Mwezeshaji wa Mafunzo hayo Jaji Mkuu Mstaafu Chande
Othmani alisema jambo muhimu kwenye usuluhishi mafanikio yake sio
nani kashinda na nani kashindwa.
Alisema kama kesi
inayokwenda mahakamani bali ni kurudisha uhusiano mwema kati ya pande
mbili zilizopo kwenye mgogoro na wao wenyewe kuweza kutatua mgogoro
wao na sio kumuachi mtu wa nje pamoja na kwamba ni mtu huru jaji au
hakimu kuweza kusuluhisha.
Alisema pia kwa sababu kuna
umuhimu wa mgogoro kusuluhishwa na wenye mgogoro wenyewe na sio mtu wa
nje ndio tofauti kubwa pili ni kwamba ili kusuluhisha ufanikiwa
lazima wale wenye mgogoro waingie kwenye usuluhushi wakiwa tayari
kutoa na kupokea kwa sababu ukiingia huko
wanaoshinda ,wanaokosa
wote lakini mahakamani ana shinda mmoja anakosa mwengine.
Aidha alisema kwenye usuluhishi wote waliopo kwenye mgogoro ni
washindi wote kila mtu anapata na katoa lazima utoe na upokee pia ni
jambo jingine muhimu kwa watanzania na Zanzibar njia moja ya kisheria
ya kutatua migogoro ni kupitia mahakama.
Jaji Mkuu
Mstaafu huyo alisema pia sheria za nchi zetu mbili pamoja na katibu ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara 107 (a) ibara ndogo2(d) inamtaka
moja katika msingi wa utoaji haki ni kutatua migogoro kwa njia mbadala
na ndio maana kwenye mashauri ya kazi kuna njia
mbadala za
kwenda kwenye Mahakama za usuluhishi (CMA).
Alisema pia
kwenye masuala la talaka ndoa kabla hujaletewa mashauri mahakamani
lazima uende kwenye bodi ya usuluhishi na ni njia mbadala ya kuweza
kutatua migogoro hiyo kwa njia ya haki mtu kupata haki kwa sababu haki
haipatikani mahakamani pekee.
Naye kwa upande wake
Mwanzilishi wa kituo cha Usuluhishi Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ,Jaji
Rose Temba alisema kituo hicho kilianzishwa ramsi kwa ajili ya
mashauri ya madai yanapopelekwa mahamakani kwa kutambua kwamba sheria
inataka usuluhi ufanyike kabla ya shauri
halijaingia kusikilizwa
rasmi .
Alisema kutokana na hilo uongozi wa mahakama
ukaona ni bora uanzishe kituo hicho ili kuwe na wataalamu ambao ni
majaji watakaokuwa na kazi yao ya kila siku ni kufanya usuluhishi na
hiyo ilitokana na ukweli kwamba majaji waliopo kwenye vituo vyao
wanafanya kazi nyingi kwa
wakati mmoja.
Alisema
unakuta wanfanya kazi za usuluhishi na kusikiliza mashauri na
kuyatolea maamuzi wakati mmoja hivyo wakaona ni jambo jema kama
kutakuwa na kituo ambacho kitakuwa ni kupoeka mashauri yaliyoiva kwa
ajili ya kufanya usuluhishi.
Hata hivyo alisema tokea
kituo hicho kimeanzishwa kumekuwa na mafanikio ndani yake maana jaji
aliyepo kwenye kituo hicho ana muda wa kutosha kuyasoma majalada na
kueleza kiini cha matatizo kabla ya wadawa hawajafika ili kuweza
kuendesha mjadala wa masuluhishio.
Naye kwa upande wake
mjumbe wa Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati
Zanzibar (ZURA) Ally Abood Mzee Mjumbe alisema wao wamepata bahati ya
kuhudhuria mafunzo hayo ya usuluhishi ambayo ni muhimu kwao kwa
kuwawezesha kujua namna ya kuweza kwenda kutatua migogoro inayokuwa
ikijitokeza.
No comments:
Post a Comment