Maofisa wa Mradi wa Best of Zanzibar wakigawa viatu kwa Watoto wa Skuli ya Msingi na Maandalizi za Kijini na Mbuyu Tende Kijiji cha Matemwe Mkoa wa Kaskazini B Unguja, uzinduzi wa uendelezaji wa kuwapitia viatu Wanafunzi, kupitia "Valisha Mtoto Viatu" hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Skuli ya Kijini Matemwe.
Best of Zanzibar inaendelea kwa mafanikio
makubwa katika Kampeni yake ya “Valisha Mtoto Viatu” katika skuli ya Kijini na
Mbuyu Tende. Kampeni hiyo yenye kutambuliwa kwa hashtag ya #PECcampaign ama kwa
lugha ya kigeni “Pair for Every Child campaign” imeweza kuwapatia watoto zaidi
ya 700 viatu kwa mwaka wa 2018. Miezi michache ya mwaka huu, Best of Zanzibar
kupitia wadau mbali mbali ndani na nje ya nchi imeweza kupata pesa za kununua
viatu ziada ya peya 400 ambavyo vitatolewa kwa watoto wa Skuli ya Maandalizi na Msingi katika Skuli za Kijini na Mbuyu Tende Matemwe.
Kupitia Kampeni hii ya viatu,
Best of Zanzibar imeweza kupunguza idadi ya watoto wanaokwenda shule bila viatu
katika vijiji hivi viwili. Watoto wadogo wa miaka minne wanatembea masafa
marefu kama kilomita 5 kwenda shule na kurudi kila siku, kipindi kama hiki cha
mvua, ama jua na ardhi hii yam awe na mavumbi ambapo inakuwa vigumu kwa watoto
hawa kuhimili.
Kampeni ya Valisha Mtoto Viatu inatoa shukurani
zake za dhati kwa wote waliofanikisha kampeni hii ndani ya Zanzibar na sehemu
nyenginezo duniani ambao wamechangia kwa lengo la kuleta mabadiliko chanya kwa
vijiji hivi vya Kijini na Mbuyu Tende.
“Lengo letu ni kuona watoto hawa wankwenda skuli
na viatu bora kwa ajili ya usalama wao na mahudhurio mazuri darsani ili
kuongeza ufanisi wao na ufaulu shuleni. Waathirika zaidi ni watoto wadogo ambao
ni chekechea na darasa la kwanza, ndio maana mwaka huu wa 2019 tumewalenga
zaidi watoto wadogo wa miaka 4 mpaka 8” Alisema Meneja wa Best of Zanzibar,
Aminata Keita. “Tunawashukuru sana wadau wetu wote na wasamaria wema kutoka
Zanzibar, Afrika Kusini na hata ghuba ya mbali (Uarabuni) ambao wamewezesha watoto
hawa kuvaa viatu. Natoa wito kwa NGO’s na mashirika mengine waungane nasi
pamoja na kufanya Kampeni hii iwezekane kwa Zanzibar nzima” Aliongezea Aminata
Keita
Mgeni Rasmi katika sherehe hiyo alikuwa ni Naibu
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar na wageni wengine mashuhuri kutoka
Serikalini na sehemu mbali mbali. Mbali na utowaji wa viatu, Best of Zanzibar
ilikabidhi zawadi kwa wanafunzi 50 ambao wamefanya vizuri katika masomo yao ya
Hisabu na Kingereza kwenye program ya masomo ya ziada ijulikanayo kama
“After-hours Tutoring Program”
“Best of Zanzibar ilianza program yake ya masomo ya
ziada kwa Kingereza na Hisabati miaka miwili iliyopita, na tunafurahi kuona
mabadiliko makubwa katika matokeo na maendeleo ya wanafunzi hawa ya mwaka 2018.
Leo tunawazawadia wanafunzi 50 waliofanya vizuri katika masomo haya mawili kwa
kuwapa mabegi ya shule vifaa vyengine vya shule. Mwaka huu, programu yetu
imeongeza walimu 6 wa masomo ya sayansi ambao nao watafanya kazi kwa
kushirikiana na walimu wakuu katika Physics, Chemistry na Biology. Tunawaomba
wanafunzi kusoma kwa bidii ili waweze kutimiza ndoto zao na kuleta mabadiliko
mazuri katika jamii yao, tunatarajia miaka ijayo Kijini itakuwa moja ya skuli
bora visiwani” Alisema Mratibu wa Elimu na Uwezeshaji wa Best of Zanzibar, Ally
Suleiman
‘Mkurugenzi wetu Bwana Brian Thomson
ameahidi kuwafadhili wanafunzi katika masomo ya Uhandisi, ijapokuwa ni vigumu
kuwapata wanafunzi wanaofaulu vizuri katika masomo ya sayansi ambalo ndio
hitajio la kwanza ili uweze kusomea Uhandisi, hii ndio sababu ya kuongeza
masomo ya sayansi kwenye program yetu” Aliongeza Ally Suleiman
“Leo tunashuhudia maadhimisho haya kwa furaha
kubwa, kupokea zawadi kwa wanafunzi wetu na viatu kwa Kampeni hii ya “Valisha
Mtoto Viatu.” Viatu hivi vimewasaidia sana wanafunzi wetu katika safari yao ya
masomo na moyo wa kuja shule. Na kuwapatia zawadi wale ambao hawakufanya sana
vizuri lakini ni wahudhuriaji wazuri zaidi na wana nidhamu nzuri, pia
itachangia kuongeza ufaulu kwani itawashawishi watoto kuja shule sasa. Wazee na
walimu wa Kijini wamefurahia watoto wao kuwa na viatu na vifaa vya shule kwa
wanafunzi zaidi ya 600 ambao wananufaika na program hii ya Best of Zanzibar,
ambayo inachangia kwa kiwango kikubwa kuleta ufanisi na matokeo mazuri kwa wanafunzi.
Mafanikio yanaonekana na tunashukuru mwaka wa pili wa watoto hawa kupata viatu”
Alisema, Mwalimu Mkuu wa Skuli ya Kijini – Ulimwengu
Shughuli hiyo iliadhimishwa na Naibu Waziri wa
Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Simai Mohammed Said, Mkuu wa Mkoa wa
Kaskazini Mhe. Vuai Mwinyi, Wakurugenzi na Viongozi wengine wa Serikali ambao
waliomba wadau wengine kuunga mkono Kampeni hiyo ya viatu sio tu kwa Kijini na
Mbuyu Tende bali kwa Zanzibar nzima.
“Tunaipongeza Best of Zanzibar kwa kuendelea na
juhudi zao za kukuza elimu Kijini na Mbuyu Tende. Wameweka mfano bora kwa
wengine kufuata kwani hakika kuwekeza kwenye elimu ni muhimu sana kwa maendeleo
ya taifa letu. Pia, natoa wito kwa wanafunzi na vijana kufanya juhudi katika
masomo yao ili waweze kufaulu, Best of Zanzibar na walimu wamefanya sehemu yao
hivyo basi na wanafunzi mfanye juhudi ili kupata mafanikio” Alisema, Hon. Simai
Said
Best of Zanzibar inawaomba wasamaria wema
kuungana nao katika Kampeni hii ya viatu na kuhakikisha watoto wote wanaenda
shule na viatu. Tuwawezeshe vijana hawa kufikia malengo yao.
Tafadhali wasiliana nasi kwa mitandao ya kijamii
au email: aminata@best-of-zanzibar.com
No comments:
Post a Comment