Habari za Punde

RAIS MHE. DKT. JOHN POMBE MAGUFULI AWEKA SHADA LA MAUA KATIKA MAKABURI YA MASHUJAA WA ZIMBABWE KATIKA ENEO LA NATIONAL HEROES ACRE WEST WING HARARE NCHINI HUMO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli akiwa mbele ya mnara wa Kumbukumbu ya Makaburi ya Mashujaa wa Taifa la Zimbabwe kabla ya kuweka shada la maua katika eneo hilo lililopo kilometa saba kutoka jiji la Harare nchini Zimbabwe.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli akiweka shada la maua mbele ya mnara wa Kumbukumbu ya Makaburi ya Mashujaa wa Taifa la Zimbabwe katika eneo hilo lililopo kilometa saba kutoka jiji la Harare nchini Zimbabwe.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli akisali mara baada ya kuweka shada la maua katika eneo hilo la makaburi ya mashujaa wa Zimbabwe.
Mnara wa Kumbukumbu katika eneo la Makaburi ya Mashujaa wa Zimbabwe kama linavyoonekana pichani. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza ujumbe wa Tanzania katika kikao na Ujumbe wa nchi ya Zimbambwe kilichokuwa kikiongozwa na Rais wa Zimbabwe Mhe.Emmerson Mnangagwa katika Ikulu ya Harare nchini Zimbabwe leo tarehe 29/05/2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli akisikiliza maelezo kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba Kabudi kuhusu Kaburi la mmoja wa Mashujaa wa Zimbabwe Herbert Wiltshire Pfumaindi Chitepo ambaye aliuwawa mwezi march 1975. Marehemu Herbert Wiltshire Pfumaindi Chitepo alikuwa Mkurugenzi wa Mashtaka DPP mweusi wa kwanza Tanganyika na Afrika.
                                                   Picha na Ikulu                                                  

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.