Habari za Punde

Vijana waaswa kutojihusisha na mambo yasiyo na tija


Na Abdalla Mfaume

Mkuu Wa Wilaya Ya Kaskazini B Ndugu Rajab Ali Rajab amewataka  vijana  kuwa wazalendo wa nchi yao  na kuachana na tabia ya kujihusisha na mambo ambayo hayana tija  yoyote.

Amesema suala la uzalendo kwa vijana ni suala muhimu na kusisitiza vijana hao kutokukubali kutumiwa na baadhi ya wanasiasa   kwa  ajili ya kutimiza malengo yao  ya kupata nafasi za uongozi na baadae kuwawacha vijana wakiwa hawajui la kufanya bila ya kuwasaidia katika kuwainuwa kiuchumi.

Kauli hiyo ameitowa wakati akifungua mafunzo ya siku moja kuhusu umuhimu wa kugombea nafasi za uongozi  kwa vijana wa shehiya za bumbwini makoba ,misufini pamoja na mafufuni  na  kusema uongozi wa wilaya katika kuwasaidia vijana kujikinga na makundi maovu umeamua kuanzisha miradi mbalimbalil ili kuwainua  vijana hao kiuchumi.


Aidha  Nd:Rajab amewataka vijana wa kike kuacha kukubali kuolewa wakati wakiwa hwajamaliza skuli  kwani  kufanya hivyo kutapelekea taifa kukosa viongozi bora wenye uzalendo na taifa lao.

Kwa upande wake mwenyekiti wa uvccm  wilaya ya mjini bi hudhaima mbarak  tahir mkufunzi wa mafunzo hayo  ameitaka jamii  kuwapa  uhuru vijana hasa   wa kike kugombea nafasi za uongozi pamoja na kuzingatia maadili ya  uongozi.

Nao baadhi ya vijana waliopata mafunzo hayo wamesema mafunzo hayo yamewaelimisha  vizuri na watagombea nafasi mbalimbali za uongozi  ili kuwatumikia wananchi katika sekta mbalimbali na wao waepukane  kutumiwa kwa ajili ya watu kupata faida.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.