Habari za Punde

Mwenge wa Uhuru Wawasili Kisiwani Pemba leo Kuaza Mbio Zake Katika Mikoa Miwili ya Pemba Ukitokea Mkoani Tanga.

MWENGE wa Uhuru ukitoka katika uwanja wa Ndege wa Pemba, kwa kutumia mchakamchaka mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Karume Pemba ukitokea Mkoani Tanga baada ya kumaliza ziara yake na kukimbizwa katika Mkoa wa Kusini Pemba
WATENDAJI mbali mbali kutoka Mkoa wa Tanga wakihudhuria katika hafla ya kukabidhi Mwenge wa Uhuru katika Mkoa wa Kusini Pemba, mwenge huo uliowasili na kaunza kukimbizwa katika Wilaya ya Mkoani.
BAADHI ya askari wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Kusini Pemba, wakiuzingia Mwenge wa Uhuru baada ya kutua katika ardhi ya Mkoa wa Kusini Pemba
MKUU wa Mkoa wa Kusini Pemba Hemed Suleiman Abdalla, akimpokea Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mzee Mkongea Ali, baada ya kuwasili Kiswani Pemba wakitokea Mkoa Tanga.
WAKUU wa Wilaya na Halmashauri za Mkoa wa Tanga, wakifuatilia kwa makini makabidhiano ya mwenge wa Uhuru kutoka Mkoa wa Tanga na Kwenda Mkoa wa Kusini Pemba, hafla iliyofanyika uwanja wa Ndege wa Karume Pemba
MKUU wa Mkoa wa Tanga Martin Rubein Shegela (kushoto), akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Hemed Suleiman Abdalla, mara baada ya kuwasili Kisiwani Pemba ukitokea Mkoa wa Tanga na kuanza kukimbizwa katika Wilaya ya Mkoani.
MKUU wa Mkoa wa Kusini Pemba Hemed Suleiman Abdalla, akisoma taarifa ya Mkoa wa huko mara baada ya kupokea mwenge wa Uhuru ukitokea Mkoa wa Tanga

MKUU wa Mkoa wa Kusini Pemba Hemed Suleiman Abdalla (Kulia), akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Issa Juma Ali na kuanza kuukimbiza katika Wilaya hiyo.(Picha na Abdi  Suleiman - Pemba)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.