Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wac Baraza la Mapinduzi Mhe,Dk. Shein Atuma Salamu za Pongezi Kwa Rais wa Misri Abd El Fattah Saeed Hussein Khalil El Sisi.


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amemtumia salam za pongezi Rais wa Jamuhuri ya Misri Abd El Fattah Saeed Hussein Khalil El Sisi, kwa kuadhimisha miaka 67 ya uhuru wa Taifa hilo.

Katika salamu zake Dk. Shein alisema kwa niaba yake , wananchi na  Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar anapongeza juhudi zinazochukuliwa na kiongozi wa Taifa hilo katika kuwaletea maendeleo wananchi wake pamoja na kuimarisha amani, umoja na mshikamano miongoni mwa nchi za Afrika, eneo la  Mashariki ya kati na duniani kwa ujumla.

Dk. Shein alisema ana matumaini makubwa kuwa juhudi zinazochukuliwa na kiongozi huyo zitakuwa chachu katika kuendeleza uhusiano mwema uliopo kati ya Zanzibar na Jamhuri ya Misri, kwa faida na maslahi ya wananchi wa nchi mbili hizo.

Aidha, Dk. Shein alitumia nafasi hiyo kumtakia afya njema na furaha kiongozi huyo pamoja na familia yake ili aweze kuendeleza amani iliopo na kukuza uchumi wa nchi hiyo.

Taifa la Jamuhuri ya Misri lilipata uhuru wake mnamo mwaka 1952 baada ya Mapinduzi ya kijeshi yalioongozwa na Mwanamapinduzi Gamel Abdel Nasser kwa kuuangusha utawala wa mabavu wa Mfalme Farouk, ambapo Jenerali Mohamed Naguib aliongoza Taifa hilo kwa mara ya kwanza.

Abdi Shamna, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax: 024 2231822 
 E-mail: abdya062@gmail.com


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.