Habari za Punde

Vilabu Vyatakiwa Kuwa Kufuata Utaratibu Uliowekwa Kuendesha Timu Zao.

Na.Mwanajuma Juma. Zanzibar.
MWENYEKITI wa Chama Cha Soka 
Zanzibar ZFF Wilaya ya Mjini Hassan Haji 
Hamza ‘Chura’ amevitaka vilabu vya soka 
nchini kufata utaratibu uliowekwa katika 
kuendesha timu 
zao ili kujiepusha na usumbufu wa kikatiba 
na kianuni.
Akizungumza katika hafla ya ufungaji wa 
mafunzo ya waalimu wa makipa wa mpira 
wa miguu mwishoni mwa wiki iliyopita 
alisema kuwa vilabu katika miaka hii 
wasitarajie mteremko kutokana na uongozi 
uliopo kuonesha kutaka mabadiliko katika 
kila kona ya 
mchezo huo.
Alisema kuwa uongozi huo mpya wameanza na kutoa mafunzo kwa waalimu wa makipa 
hatua ambayo inaonekana itaendelea kwa kada zote zinazohusu soka.
“Napenda kusema kuwa inaonekana sasa Zanzibar inabadilika na kuelekea kule ambapo 
tunataka na kwa hatua hii karibuni baadhi ya vilabu vingi vitakufa kutokana na watu ambao 
wamekuja kusimamia misingi na kanuni za soka”, alisema.
Hivyo alisema kuwa kwa wale ambao wamekuwa wakionekana kuongoza kimazoea 
wataweza kukaa pembeni kutokana na kuja kuona kwamba wanaonewa pale ambapo 
watatakiwa wafate taratibu.
Aidha alifahamisha kwamba taaluma ni muhimu sana kwa sababu vilabu vingi 
vimekuwa wakiwaacha nyuma makipa kutokana na kile alichodai kukosa wasimamizi.
Hivyo alisema kuwa kufatia hatua hiyo itawafanya na wao waweze 
kutambulika na kupatiwa waalimu wa kuwafundisha ambao wataweza kuwatoa makosa yao 
pale wanapokosea kama ambavyo ilivyo kwa wachezaji wengine.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.