Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Mitihani Tanzania Dkt. Charles E. Msonde, akisisitiza jambo wakati akizungumza na Waandishi wa habari wa Vyombo mbalimbali vilioko Zanzibar, akitowa matokea ya Mitihani ya Taifa ya Kidatu cha Sita kwa mwaka huu, Mei 2019, katika ukumbi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mazizini Zanzibar.
Na.Mwanajuma Juma. Zanzibar.
JUMLA ya wanafunzi wapatao 88,069 wamefaulu mitihani yao ya kidato cha sita ikiwa ni sawa na asilimia 98.32 ya watahiniwa waliofanya mitihani.
Matokeo ya mitihani hayo yalitangazwa jana na Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani
Tanzania Dkt. Charles Enock Msonde mbele ya waandishi wa habari na kusema kuwa
ufaulu wa mwaka huu umeongezeka kwa asilimia 0.74.
Alisema kuwa kati ya wanafunzi hao waliofaulu wasichana ni 37,219 sawa na asilimia
99.11 na wavulana ni 50,581 sawa na asilimia 97.75 .
Aidha alisema kuwa katika matokeo hayo watahiniwa wa shule waliofaulu ni 78,666
sawa na asilimia 99.14 ya waliofanya mitihani na watahiniwa wa kujitegemea ni 9,403 ikiwa
ni sawa na asilimia 91.95 .
Alifahamisha kwamba juma la wanafunzi 91,298 walisajiliwa kufanya mtihani huo
wakiwemo wasichana 37,948 sawa na asilimia 41.56 na wavulana 53,350 sawa na
asilimia 58.44 ambapo watahiniwa 90,001 sawa na asilimia 98.58 walifanya mtihani na
watahiniwa 1,297 sawa na asilimia 1.42 hawakufanya mtihani kutokana na sababu
mbali mbali zikiwemo za ugonjwa na utoro.
Aidha alieleza kuwa ubora wa ufaulu kwa kuangalia madaraja waliyopata watahiniwa
wa shule unaonesha kuwa jumla ya watahiniwa 76,655 sawa
na asilimia 96.61 wamefaulu katika daraja la kwanza hadi la tatu wakiwemo wasichana
32,887 sawa na asilimia 97.22 na wavulana 43,768 sawa na asilimia 96.15.
Hata hivyo alisema kuwa takwimu za ufaulu kwa watahiniwa wa shule wa mwaka huu,
ikilinganishwa na mwaka jana zinaonesha kuwa ufaulu katika masomo ya Geography,
Kiswahili, Engilish Language, French Language, Kiarabu, Basic Applied Mathematics,
Advance Mathematics, Economics na Food anda Human Nutrition umepanda
ikilinganishwa na mwaka jana.
Aidha alisema kuwa ufaulu katika masomo ya General Studies, History, Biology na
Acountance umeshuka kidogo ikilinganishwa na mwaka 2018 .
Aidha Baraza ka Mitihani limefuta matokeo yote ya watahiniwa 14 waliobainika kufanya
udanganyifu katika mitihani yao kati ya hao tisa ni watahiniwa wa shule na watano ni
watahiniwa wa kujetegemea.
SHULE 10 BORA KITAIFA
Kisimiri ya Arusha, Feza Boys Dar Es Salaam, Ahmes ya Pwani, Mwandet ya Arusha,
Tabora Boys Tabora, Kibaha Pwani, Feza Girls ya Dar Es Salaam, ST.Mary’s Mazinde
Juu, Canossa ya Dar Es Salaam na Kemebos ya Kagera.
SHULE 10 ZA MWISHO KITAIFA
Nyamunga ya Mara, Haile Selassie mjini Magharibi, Tumekuja Mjini Magharibi, Bumangi ya Mara, Buturi ya Mara, Mpendae Mjini Magharibi, Eckernforde Tanga, Nsimbo Katavi,
Mondo ya Dodoma na Kiembesamaki A Islamic ya Mjini Magharibi.
WATAHINIWA 10 BORA KITAIFA KWA MASOMO YA SAYANSI
Faith Nicholous Matee (ST. Mary’s Mzinde Juu Tanga), Herman Pauline Kamugisha (Kisimiri Arusha),
Levina Calist Chami (ST. Coreti ya Kilimanjaro),
Benius Eustace (Mzumbe ya Morogoro),
Augostino Issaya Omari (Ilboru ya Arusha),
Satrumin Arbogast Shirima (Temeke Dar Es Salaam),
Khalid Hussein Abdalla, (Feza Boys Dar Es Salaam),
Levina Calist Chami (ST. Coreti ya Kilimanjaro),
Benius Eustace (Mzumbe ya Morogoro),
Augostino Issaya Omari (Ilboru ya Arusha),
Satrumin Arbogast Shirima (Temeke Dar Es Salaam),
Khalid Hussein Abdalla, (Feza Boys Dar Es Salaam),
Assad Y.Msangi (Feza Boys Dar Es Salaam),
Peter Jovenal Riima (Kibaha Pwani) na
Peter Jovenal Riima (Kibaha Pwani) na
Augustine J. Kamba (Feza Boys ya Dar E Salaam).
WASICHANA 10 BORA MASOMO YA SAYANSI
Faith Nicholous Matee (ST. Mary’s Mzinde Juu Tanga), Levina Calist Chami (ST. Coreti ya Kilimanjaro),
Wahida Janguo (Feza Girls Dar Es Salaam),
Vanessa R. Rutabana (Tabora Girls ya Tabora),
Pielina M. Figowole (Tabora Girls ya Tabora),
Loveness Samson Mloge (ST. Mary’s Mzinde Juu), Wahida Mbaraka Uzia (Zanzibar Feza Mjini Magharibi), Beatrice Martin Mwella (St. Mary’s Mzinde Juu),
Consolata Seraphin Matee (St. Mary’s Mzinde Juu) na Maimuna A. Mshana (Marian Girls ya Pwani).
Wahida Janguo (Feza Girls Dar Es Salaam),
Vanessa R. Rutabana (Tabora Girls ya Tabora),
Pielina M. Figowole (Tabora Girls ya Tabora),
Loveness Samson Mloge (ST. Mary’s Mzinde Juu), Wahida Mbaraka Uzia (Zanzibar Feza Mjini Magharibi), Beatrice Martin Mwella (St. Mary’s Mzinde Juu),
Consolata Seraphin Matee (St. Mary’s Mzinde Juu) na Maimuna A. Mshana (Marian Girls ya Pwani).
WAVULANA 10 BORA KITAIFA MASOMO YA SAYANSI
Herman Pauline Kamugisha (Kisimiri Arusha), Benius Eustace (Mzumbe ya Morogoro), Augostino Issaya Omari (Ilboru ya Arusha), Satrumin Arbogast Shirima (Temeke Dar Es
Salaam), Khalid Hussein Abdalla, (Feza Boys Dar Es Salaam), Assad Y.Msangi (Feza Boys
Dar Es Salaam), Peter Jovenal Riima (Kibaha Pwani) na Augustine J. Kamba (Feza Boys ya
Dar E Salaam).Shedrack Leonartus Siame (UWATA Mbeya) na Noel Godwin Maro (ST.
Mary Goreti Kilimanjaro).
WATAHINIWA 10 BORA KITAIFA LUGHA NA SANAA
Victor Mtui (Feza Boys Dar), Paula Nelson Lujwanga na Blandina Kessy Nyange (St. Mary Mzinde Juu Tanga), Eva J. Shitindi (Machame Girls Kilimanjaro), Ruhinda Benedicto
Machimu (St. Mary Mzinde Juu Tanga), Anita Zacharia Massawe (ST. Mary’s Mzinde Juu
Tanga), Karrim Kassimu Muhibu (Nyangao Lindi), Anold Andrea Msuya (Dareda Manyara), Latifa Mohammed Mrosso (Ahmes Pwani) na Elibariki Desidery Baliyanga (Lukole Kagera).
WASICHANA 10 BORA KITAIFA LUGHA NA SANAA
Paula Nelson Lujwangana, Blandina Kessy Nyange (St. Mary Mzinde Juu Tanga), Eva J. Shitindi (Machame Girls Kilimanjaro), Anita Zacharia Masawe (St. Mary Mzinde
uu Tanga), Latifa Mohammed Mrosso (Ahmes Pwani), Mwanakombo Yussuf Ramadhan
(Mtwara Girls Mtwara), Katarina Damas Shao (Kisimiri Arusha), Pakusana Henry Chaula (St. Mary’s Mzinde Juu Tanga), Minnah K. Mtingwa (Feza Girls Dar) na Jasintha
Deogratias (Lukole Kagera).
WAVULANA 10 BORA KITAIFA MASOMO YA LUGHA NA SANAA
Victor Mtui (Feza Boys Dar), Rushinda Benedicto Machimu (St. Mary Mzinde Juu Tanga), Karrim Kassimu Muhibu (Nyangao Lindi), Elibariki Desidery Baliyanga (Lukole Kagera).
Joseph Anold Andrea Msuya (Dareda Manyara), Joseph Kelvin Komba (Kisimiri Arusha),
Malugu M. Maganyala (Feza Boys Dar), Daudi Mbukwa (Kisimiri Arusha), Frank J.
Mwampembe na Paschal K. Nhumba (Lukole Kagera).
WATAHINIWA 10 BORA KITAIFA BIASAHARA
Noreen M. Lyimo (Baobab Pwani), Aston Stevin Ngaeje (Kibaha Pwani), Doreen A. Lipamba (Benjamin Willium Mkapa Dar), Emmanuel P. Chila (Alpha Dar), Mery D. Samwel na
Glory Danny Kandonga (Weruweru Kilimanjaro), Merciana A. Msechu (Mpanda Girls
Katavi), Getruda Didoris Ndongo (ST. Christina Girls Tanga) na Athumani Magadura
Willium (Umbwe Kilimanjaro).
WASICHANA 10 BORA KITAIFA BIASHARA
Noreen M. Lyimo (Baobab Pwani), Doreen A. Lipamba (Benjamin Willium Mkapa Dar), Mery D. Samwel na Glory Danny
Kandonga (Weruweru Kilimanjaro), Merciana A. Msechu (Mpanda Girls Katavi),
Getruda Didoris Ndongo (ST. Christina Girls Tanga), Irene Ishael Barakaeli (Nganza
Mwanza), Rahel P. Kyokola (St. Mary Goreti Kilimanjaro), Salma A. Shekimweri (Kibasila
Dar) na Grace Hayrod Ng’ondya (Weruweru Kilimanjaro).
WAVULANA 10 BORA KITAIFA BIASHARA
Aston Stevin Ngaeje (Kibaha Pwani), Gift Mwakikusi (Tusiime Dar), Emmanuel P. Chila (Alpha Dar), Athumani Magadura Willium (Umbwe Kilimanjaro), Stephano Y.
Dismas (Kibaha Pwani), Robert John Tano (Scolastica Kilimanjaro), Dotee A. Zuberi
Galanos Tanga), Ernest P. Game (Kibaha Pwani) na Deogratias Ladislaus Msilanga
(Kibaha Pwani).
Hata hivyo alisema kuwa ubora wa ufaulu umezidi kuimarika kwa kuwa na idadi ya
watahiniwa waliofaulu vizuri katika daraja la kwanza hadi la tatu imeongezeka kwa
asilimia 1.09kutoka asilimia 95.52 ya mwaka 2018 na kuwa asilimia 96.61 ya mwaka 2019.
Aidha alisema kuwa ubora wa ufaulu wa wasichana kwa mwaka 2019 umezidi ule wa
wavulana kwa asilimia 1.07.Sambamba na hayo alisema kuwa Baraza la Mitihani Tanzania
lilifanya uchambuzi wa kina wa matokeo hayo kwa kila somo na kutoa machapisho ya
uchambuzi huo yakatakayowasilishwa kwa wadau wa elimu zikiwemo shule zote za
Sekondari za Juu (‘A’ Level) nchini kwa lengo la kuwezesha walimu kutumia taarifa za
uchambuzi katika kuboresha ufundishaji na ujifunzaji shuleni.
Hata hivyo katika matokeo hayo watahiniwa 20 wa shule ambao walipata matatizo ya
kiafya na kushindwa kufanya mitihani kwa baadhi ya masomo yamezuiliwa matokeo
hayo na watahiniwa hao wamepewa fursa ya kufanya mitihani yao hiyo Mei mwakani
kama watahiniwa wa shule.
Dkt. Msonde alisema kuwa Baraza linapenda kuchukuwa fursa hizo kuzipongeza kamati za
Uwendeshaji Mitihani za mikoa na Halmashauri /Manispaa//Majiji nchini, Wakuu
wa shule na wasimamizi wa mitihani kwa kuzingatia na kusimamia taratibu
za uwendeshaji mitihani na hivyo kuzuia kwa kiasi kikubwa udanganyifu kufanyika.
No comments:
Post a Comment