RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein leo amefanya uteuzi wa viongozi katika taasisi mbali mbali za
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Walioteuliwa ni Ali
Khamis Juma kuwa Mkurugenzi wa Jiji la Zanzibar katika Ofisi ya Rais, Tawala za
Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ.
Mwengine ni Khadija
Khamis Rajab ameteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu katika Wizara ya Biashara na
Viwanda, Hanifa Ramadhani Said ameteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Msaada wa
Kisheria katika Wizara ya Katiba na Sheria.
Masoud Ali Mohamed
ameteuliwa kuwa Ofisa Mdhamini Pemba katika Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na
Utawala Bora na Mattar Zahor Masoud ameteuliwa kuwa Ofisa Mdhamini Pemba katika
Wizara ya Katiba na Sheria.
Aidha, Rais Dk. Shein
amemteua Dk. Haji Ali Haji kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wakala wa
Mkonga wa Mawasiliano wa Zanzibar katika Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji.
Pia, Rais Dk. Shein
amemteua Shukuru Awadh Suleiman kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Mkonga wa
Mawasiliano wa Zanzibar katika Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji.
Kwa mujibu wa Taarifa
iliyotolewa kwa vyombo vya habari na kusainiwa
na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Dk. Abdulhamid Yahya
Mzee, uteuzi huo umeanza rasmi leo tarehe 6 Agosti, 2019.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment