Habari za Punde

Ligi Daraja la Kwanza Unguja kwa Mwaka 2019/2020 Kutimua Vumbi Kesho Zanzibar.


Na Hawa Ali, Zanzibar. 
Ligi daraja la Kwanza Kanda ya Unguja inatarajia kuanza kutimua Vumbi jumaa tatu hii  msimu mpya wa mwaka 2019-2020. 

Jumla ya Michezo mitatu inatarajiwa kupigwa katika viwanja tofauti ambapo  Bweleo na Dula Boys watakipiga uwanja wa Mao A, wakati Miembeni na Kikwajuni watapepetana katika kiwanja cha Mao B, huku watembeza watalii wa Nungwi timu ya Mundu watajitupa uwanja wa Amaan wakiminyana na timu ya Uhamiaji. 

Akizungumza na Gazeti hili Mkurugenzi wa Kamati ya Mashindano ya ZFF Ali Mohammed alisema ligi ya msimu huu itakuwa ya namna yake ikiwemo hata mabadiliko ya Viwanja vya kucheza. 

Alisema msimu huu katika kuboresha ligi hiyo  imeona ipo haja ya kutumia viwanja vilivyopo  mji wa Zanzibar ikilinganishwa msimu iliyopita ambapo mechi nyingi zilikuwa zikichezwa katika viwanja vya mashamba hali iliyopelekea hata kuongeza kwa wimbi la kupigwa Waamuzi. 

Alisema msimu huu ligi daraja  Kanda kwa kuanzia vitatumika viwanja viwili tu ambavyo  ni kiwanja cha Amaan na kiwanja cha Mao ze dong Ili kupunguza malalamiko yanayotolewa na Waamuzi ikiwemo kupigwa na viongozi wa vilabu na hata mashabiki pindi wanapochezesha katika viwanja ambavyo walidai havina ulinzi wa kutosha.

“Msimu huu tutaanza na viwanja viwili kwanza huku tukiangalia mpaka dilisha dogo kama tutaongea viwanja vingine au tutatumia hapo hapo Mau na Amaan na tayari tushawaita viongozi wa vilabu tumezungumza nao juu ya mabadiliko haya ya Viwanja na wao wameelewa"Alisema

Ligi hiyo inatarajia kushirikisha timu 13 ambazo ni Kikwajuni, Miembeni, Taifa ya Jang'ombe, Mwembe Makumbi City, Bweleo, Dula Boys, Mchangani United, Mundu, Kilimanicity, Uhamiaji, Idumu, na Blak sailor

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.