Habari za Punde

Uzinduzi wa Kuwasili Kwa Ndege ya Rossiya Airline Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar Ikiwa na Watalii 523 Wakitokea Nchi Urusi.

Ndege ya Shirika la Rossiya Airline ikiwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar ikipokelewa kwa heshima na kumwagiliwa maji na gari za Kikosi cha Zimamoto Zanzibar ikiwa ni ishara ya mapokezi ya ndege hiyo iliozindua Safari yake leo Zanzibar ikiwa na Watalii 523 wakiwasili Zanzibar kutembelea Vivutio vya Utalii Kisiwani Zanzibar.Rossiya Air line itafanya Safari zake mari mbili katika wiki kati ya Zanzibar na Urusi.


Waziri wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar.Mhe.Mahmoud Thabit Kombo akikata Utepe kuashiria kuzindua Safazi za Ndege ya Rossiya Airline,wakati wa kuwasili kwa Ndege hiyo kubwa ya Boing 747, ikiwa na Watalii 523 kulia Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Viwanja Vya Ndege Zanzibar (ZAA)  Ndg. Hamdani Omar Makame, Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Sans Frontieres Tourism.Mr.Abu Hassan na kushoto Naibu Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji.Mhe. Mohamed Ahmad Salum, wakishiriki katika hafla hiyo ya Uzinduzi wa Safari za Ndege za Shirika la Rossiya Airline.uliofanyika leo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar.  
Waziri wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar.Mhe.Mahmoud Thabit Kombo akipiga makofi baada ya kukata utepe kuashiria kuzindua Safazi za Ndege ya Rossiya Airline,wakati wa kuwasili kwa Ndege hiyo kubwa ya Boing 747, ikiwa na Watalii 523 kulia Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Viwanja Vya Ndege Zanzibar (ZAA)  Ndg. Hamdani Omar Makame, Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Sans Frontieres Tourism.Mr.Abu Hassan na kushoto Naibu Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji.Mhe. Mohamed Ahmad Salum, wakishiriki katika hafla hiyo ya Uzinduzi wa Safari za Ndege za Shirika la Rossiya Airline.uliofanyika leo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar.  

















No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.