Habari za Punde

WAPUUZENI WANAOPINGA MPANGO WA VIFURUSHI - RC GAMBO


Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mhe. Anne Makinda akiongea na Wakazi wa Arusha wakati wa Uzinduzi wa kampeni za kuhamasisha wananchi kujiunga na mpango wa Vifurushi vya Bima ya Afya Mkoani Arusha, ambapo alisema aliwataka watanzania iwapo akifanya kazi matumizi ya kwanza iwe afya yako, na kuwataka kutoweka rehani maisha yao, kwani hautaweza kuwa na maendeleo kama hauna uhakika wa huduma za matibabu


Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo akitoa kadi za bima ya afya kwa baadhi ya wakazi wa Arusha waliojiunga na mpango wa Vifurushi vya Bima ya Afya, wakati wa Uzinduzi wa kampeni za kuhamasisha wananchi kujiunga na mpango wa Vifurushi vya Bima ya Afya Mkoani humo.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Bw. Mrisho Gambo amesema kuwa wanaopinga utaratibu wa vifurushi vya bima ya afya hawawatakii mema watanzania.

Hayo ameyasema leo wakati akizindua mpango wa uhamasishaji wa wananchi kujiunga na NHIF kupitia vifurushi vipya katika soko la Mbauda jijini Arusha.

"Ukisikia mtu anapinga mpango huu hakutakii mema kwani pindi unapopatwa na matatizo hatakuja kukusaidia hivyo tuwapuuze na tujiunge na mapango huu wa bima ya afya," alisema Mhe. Gambo.

“Gharama za matibabu kwasasa ni kubwa sana, unaweza kwenda hospotali gharama za matibabu zikawa ni kubwa kuliko kifurushi cha bima ya afya, ndugu zangu tujiunge na mpango huu ili tuwe na uhakika wa matibabu wakati wowote”-Alisisitiza Mhe. Gambo.

Kutokana na umuhimu huo amewataka  viongozi wa mkoa pamoja na viongozi wa dini kushirikiana kwa pamoja katika kuwahimiza na kuwakumbusha wananchi juu ya kuwa na bima ya afya.

Alisema mpango  wa vifurushi vya bima ya afya unamwezesha mwananchi kupata tiba popote pale nchini bila ya usumbufu wowote.

"Bima ya Afya chini ya uenyekiti wa Mhe. Mama Anne Makinda imekuwa ni bima ya afya iliyoimara sana, nakupongeza sana kwa kazi kubwa uliyoifanya wewe na bodi yako," alisema.

Alisema kuwa pamoja na Serikali ya Awamu ya Tano kuboresha Mfumo wa Bima ya Afya pia imeendele kuboresha miundombinu ya maeneo ya kutolea huduma ili mwananchi  anapokuwa na kadi yake ya bima anakuwa na uhakika wa matibabu na yenye kiwango bora.

"Mimi ni balozi mkubwa sana wa mpango huu wa bima ya afya kwasababu najua umuhimu wake hasa wakati mtu anapopatwa na maradhi, unapokuwa na kadi unakuwa na amani ndani ya familia yako wakati wote," alisema.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya NHIF, Mama Anne Makinda amesisitiza wananchi juu kuweka kipaumbele katika suala zima la bima ya Afya ndani ya familia zao.

"Ukifanya kazi matumizi ya kwanza iwe afya yako, tusiweke rehani maisha yetu, hautaweza kuwa na maendeleo kama hauna uhakika wa huduma za matibabu," alisema Mama Makinda.

Alisema kuwa kadi ya vifurushi inamuwezesha mwanachama kupata huduma za matibabu popote anapokuwa ndani ya nchi.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.