Habari za Punde

T-MARC TANZANIA YATOA MSAADA WA TAULO ZA KIKE ZA FLOWLESS, SEKONDARI YA MUGABE DAR ES SALAAM

Mkurugenzi wa Bidhaa za Kijamii wa T-MARC Tanzania, Flavian Ngole, akiongea na wanafunzi wa kike wa sekondari ya Mugabe wakati wa hafla ya kukabidhi taulo za kike kwa wanafunzi wa shule hiyo.
 Mkurugenzi wa Bidhaa za Kijamii wa T-MARC Tanzania,Flavian Ngole (kushoto) akikabidhi taulo za kike kwa Mwalimu mlezi wa shule ya sekondari ya Mugabe iliyopo Sinza jijini Dar es Salaam, Theresia Paulo, wakati wa hafla ya hafla ya kukabidhi msaada wa taulo za kike zilizozinduliwa na taasisi hiyo nchini zinazojulikana kama Flowless, wa pili kushoto ni balozi wa bidhaa hiyo, Dinnah Marrios.
Mkurugenzi wa Bidhaa za Kijamii wa T-MARC Tanzania, Flavian Ngole, (kushoto) akikabidhi taulo za kike kwa mmoja wa wanafunzi wa shule ya sekondari ya Mugabe iliyopo wilayani Kinondoni,Judith Michael, wakati wa hafla ya kukabidhi msaada wa taulo za kike zilizozinduliwa na taasisi hiyo nchini zinazojulikana kama Flowless, kwa wanafunzi wa shule hiyo ,wa pili kushoto ni balozi wa bidhaa hiyo, Dinnah Marrios.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.