Habari za Punde

Wateja wa Zantel kununua tiketi za boti za ZanFast Ferries kwa Ezypesa


Mkuu wa Zantel- Zanzibar, Mohammed Mussa akizungumza na wadau mbalimbali wakati Kampuni hiyo ilipoingia makubaliano na Kampuni ya Vigor Group wamiliki wa boti za ZanFast Ferries ili kuwawezesha wateja kununua tiketi kirahisi zaidi kwa njia ya Ezypesa.Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Vigor Group, Abdallah Turky na baadhi ya watendaji kutoka Kampuni hizo mbili.Hatua hiyo inatarajia kuboresha upatikanaji wa huduma kwa wasafiri wa ndani na nje.
Mkuu wa Masoko na Huduma za Kifedha wa Zantel, Sakyi Opoku akipeana mkono na Mkurugenzi Mtendaji wa Rahisi Solutions, Abdirahman Hassan baada ya Kampuni hizo kuingia ubia ili kuboresha huduma za mawasiliano kwa kuwawezesha wateja kununua tiketi rahisi zaidi kwa Ezypesa.Huduma hiyo ni ya kwanza nchini kutoka Zantel.Kulia ni Mkuu wa Zantel-Zanzibar, Mohammed Mussa.  

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Vigor Group, Abdalkah Turky akizungumza na wadau mbalimbali wakati kampuni hiyo ilipoingia makubaliano na Kampuni ya mawasiliano ya Zantel ili kuwawezesha wateja wake kununua tiketi kwa njia ya Ezypesa.Kulia ni Mkuu wa Zantel Zanzibar-Mohammed Mussa na Kaimu Afisa wa fedha Zantel, Aziz Ali.

Wateja waZantel wataweza kununua tiketi za usafiri wa boti za ZanFast Ferries kwa urahisi zaidi kwa kulipa kwa Ezypesa baada ya kampuni hiyo kuingia ubia na Kampuni ya usafirishaji ya Vigor Group ambayo inamiliki boti za ZanFast Ferries ili kuboresha huduma za ukataji tiketi kwa wateja wao.

Kampuni hiyo ni moja ya watoa huduma za usafiri wa majini kati ya Zanzibar na Dar es Salaam zinazochangia katika urahisishaji wa huduma za usafiri kwa wenyeji na wageni.

Akizungumzia hatua hiyo, Mkuu wa Zantel-Zanzibar, Mohammed Mussa alisema hatua hiyo imelenga kurahisisha upatikanaji wa huduma za ukataji tiketi kwa abiria hivyo kuboresha maisha ya wateja wao.

“Kwa kupitia Ezypesa tunahakikaisha wateja wanafanya malipo yao kwa urahisi zaidi,mahali popote na wakati wowote.Ushirikiano wetu naZanFast Ferries unawapa wateja uhuru zaidi wa kununua tiketi na kupunguza muda na mchakato wa kununua tiketi,” alisema Mussa.

Ili kupata tiketi, mteja wa Zantel atatakiwa kupakua application ya ZanFast Ferries kishanenda Kata tiketi,chagua Ezypesa na fanya malipo.Baada ya kukamilisha malipo mteja atapokea ujumbe mfupi (SMS)  Pamoja na tiketi laini (e-ticket) itakayotumika siku ya safari.

“Tunaamini njia hii ni suluhu ya muda mrefu na itaboresha namna wateja wanavyopata huduma za usafiri hususan wasafiri wa ndani kwani kwa sasa hakuna haja ya kwenda tena katika ofisi bali ukiwa na simu yako tu unaweza kujihakikishai uhakika wa kupata usafiri,” alisema Mkuu wa Masoko na Huduma za Kifedha wa Zantel, Sakyi Opoku.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Vigor Group, Abdallah Turky alisema kampuni hiyo imejidhatiti katika kuboresha huduma za usafiri kwa kuhakikisha inawapa wateja njia rahisi na za kidigitali za kufanya malipo ya tiketi.

“Ushirikiano baina yetu na Ezypesa umetanua wigo wa njia za malipo sanjari na App yetu ya ZanFast Ferries ambazo zinampa mteja uhuru wa kununua tiketi mahali popote alipo,” alisema.

Aliongeza kuwa kampuni hiyo itaendelea kushirikiana na Zantel katika kuleta huduma na bidhaa za kidigitali ili kurahisisha malipo kwa wateja wake.

Wateja watakaofanya malipo kwa Ezypesa watatumia tiketi laini (e-ticket) badala ya tiketi za kawaida na watatakiwa kuwa nayo siku ya safari.

Kuhusu Zantel

Zantel ni Kampuni inyaoongoza kwa utoaji wa huduma za mawasiliano Visiwani Zanzibar kwa miaka mingi hivi sasa ikiongoza kwa ubora miundombinu ya mawasiliano, huduma pamoja na bidhaa.

Huduma ya kifedha ya Ezypesa ni ya kwanza nchini Tanzania kutoa huduma za kibenki za kawaida pamoja na za kiislamu kwa ushirikiano na benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ).

Aidha, Zantel ni kampuni inayoongoza kwa utoaji wa huduma za intaneti nchini Tanzania kupitia uwekezaji kwenye teknolojia ya fibre optic cable ambayo inaiunganisha Tanzania na nchi nyingine za Afrika Mashariki na duniani umeiwezesha Kampuni hiyo kuleta mapinduzi ya haraka ya kidigitali hapa nchini.

Aidha,Miundombinu hiyo  imeiwezesha Zantel kutoa huduma za kimataifa za sauti na data kwa jumla kwa kampuni nyingine na nchi jirani hivyo kuchagiza ukuaji wa teknolojia ya digitali.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.